KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 6, 2016

WAKURUGENZI WATAKIWA KUWALIPA POSHO ZA SARE WAUGUZI

kii1
Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu,akiongea na wauguzi(hawapo pichani)wakati wa ufunguzi wa mkutano wa 44 wa wauguzi Tanzania
Na. Catherine Sungura,WAMJW -Kigoma
Wakurugenzi wa Halmashauri na wale wa hospitali za umma nchini wamepewa siku sitini kuanzia jana wawe wamewalipa posho za wauguzi za kununua sare za kazi ya shilingi laki moja na elfu ishirini pamoja na malimbikizo ya sare hizo.
Agizo hilo limetolewa mkoani hapa na Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa 44 wa wauguzi Tanzania.
Waziri Ummy alisema asilimia themanini ya kazi zote  kwenye sekta ya afya nchini zinafanywa na wauguzi,hivyo aliwataka wakurugenzi  kuzingatia miongozo iliyopo ya Serikali, “kama mwongozo ni kulipa elfu thelatini lipa thelathini si  vinginevyo. Serikali imekwishatoa waraka wa kazi za ziada yaani “extra duty circular” ambao unapaswa kufuatwa hata mnapofanya kazi usiku kwani kuna masaa ya ziada”. 
“Nawaagiza waajiri wote kuzingatia nyaraka hizi ili kuondoa malalamiko yasiyo ya lazima, Hili ni suala muhimu kwani mnakuwa kazini siku tano hadi sita kwa wiki hivyo mnahitaji sare walau tano ili muweze kubadilisha kila mara. Serikali itatoa waraka wa si chini ya laki tatu kulingana na hali ya uchumi itavyokuwa. Natumaini waraka huu utatoka mapema na kuanza kutumika mwaka ujao wa fedha hivyo kwa mwaka huu tuendelee kutumia waraka uliopo. 
Aidha, aliagiza baada ya siku sitini alizotoa kupatiwa orodha  za halmashauri ambazo hazitokuwa zimewalipa posho hizo na mikoa ipi”kwani kuna wauguzi wangapi hadi mshindwe kuwapa posho za sare ,mnataka wauguzi hawa waje kazini wawe wamevaa nini?aliuliza Waziri
Akijibu tatizo la kusimamishwa na kufukuzwa kazi kwa wauguzi na wakunga alisema ,suala la kusimamisha au kumwachisha kazi mtumishi lina taratibu zake ambazo zinapaswa kufuatwa. “Napenda kuliagiza Baraza la Wauguzi na Wakunga Tanzania kuwaelimisha waajiri kuhusu hatua za kufuata katika kushughulikia malalamiko yanayotolewa na wananchi ili yaweze kusikilizwa kwa utaratibu zilizopo bila ya kuwaonea pande zote, Ni kweli kuwa unapoadhibiwa bila kosa inavunja moyo, Naomba ieleweke kuwa sio nia ya Serikali kuwaumiza wauguzi bali lengo letu kubwa ni kuondoa kero za wananchi ikiwa ni pamoja na kuwashughulikia watumishi wote wazembe na wasiofuata maadili ya kazi”.

No comments:

Post a Comment