KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 31, 2016

WAPINZANI WATAKIWA KUSIFU MAZURI YA SERIKALI

indexNa Masanja Mabula –Pemba
 
VIONGOZI wa vyama vya upinzani hapa nchini  wametakiwa kuacha kusema mabaya Serikali pekee , bali wajenge utamaduni ya kuisifu na kuipongeza Serikali pale inapofanya jambo la maendeleo kwa wananchi wake .
 
Naibu Katibu Mkuu wa UDP Zanzibar Juma Khamis Faki amesema kwamba uwepo wa vyama vya upinzani ni kuikosoa  Serikali lakini pale inapofanya jambo la maendeleo ni wajibu wao pia kuipongeza.
 
Akizungumza na wandishi wa habari Kisiwani Pemba , Juma alisema baadhi ya wanasiasa wa upinzani wanashindwa kutambua dhana ya demokrasia kwani wamekuwa wakiitumia kupandikiza mbegu za chuki miongoni mwa wananchi .
 
Alisema kitendo kinachofanywa na baadhi ya viongozi wa vyama vya upinzani kinawajenga wafuasi wao kuamini kwamba maendeleo ya kweli yanaweza kuletwa na wao jambo ambalo wanalifanya kwa ajili ya kujitafutia umaarufu .
 
Aidha alieleza kuwa  katika kipindi hichi cha uongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ya awamu ya saba pamoja na ile ya Jamhuri ya Muungano ya awamu ya tano zimewafanyia mambo mengi wananchi , hivyo ni jukumu la wanasiasa kupanda kwenye viriri na kuyachambua moja baada ya jengine .
 
“Ni vyema viongozi wa vyama vya upinzani tukajenga utamaduni wa kuyatumia majukwaa ya kisiasa kuwaeleza wananchi ukweli na uhalisia ya mambo yanayofanywa na Serikali zao , tuacheni kasumba na kukosoa kila kitu hata kama ni cha maendeleo ”alisema .
 
Alizidi kusema “Serikali za CCM zilizopo madarakani kwa hivi sasa zimewafanyia mambo mengi wananchi ikiwemo barabara  , afya, elimu , maji na nishati ya umeme lakini wapinzani hatuyasemi , tuwaambieni ukweli wananchi na tusijitafutie umaarufu wa kisiasa tu palipo na ukweli lazima usemwe ”aliongeza.
 
Katika hatua nyingine Naibu Katibu huyo aliwashauri Viongozi wa CCM kuanzia Jimbo hadi Mkoa kuwahamasisha wajumbe wa baraza la wawakilishi kufanya kazi katika majimbo hayo ili kuleta utofauti kati ya waliowatangulia .
 
Alisema wananchi walikuwa  na matumaini ya mabadiliko ya maendeleo ndani ya majimbo yao mara baada ya uchaguzi , lakini baadhi ya viongozi hao wameyahama majimbo na kuyatelekeza na kushindwa kutimiza ahadi walizozitoa.

No comments:

Post a Comment