
Waziri wa Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na WatotoMh. Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi
wa habari wakati alipokuwa akitoa tamko la serikali kuhusu Takwimu za
viashiria vya Ukimwi na Maralia mwaka 2011-2012 na kiwango cha
maambukizi ya Ukimwi (VVU) kushoto kwake ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Bakari Kambi.
……………………………………………………………………
Kwa mujibu wa Takwimu za
Viashiria vya UKIMWI na Malaria za mwaka 2011-2012, kiwango cha
maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) nchini kinakadiriwa kuwa ni
asilimia 5.1 miongoni mwa watu wazima wenye umri kati ya miaka 15 – 49.
Takwimu hizi zinaashiria kwamba, kwa kila watanzania 1000, watu 51
miongoni mwao wanaoishi na maambukizi ya VVU. Inakadiriwa kuwa, kuna
watu 1,400,000 wanaishi na VVU nchini Tanzania ambapo, watu 839,574
wanapatiwa tiba ya dawa za kupunguza makali ya VVU zinazotolewa katika
vituo 4,000 vilikuwa vinatoa huduma hiyo nchi nzima hadi kufikia mwezi
Juni mwaka huu (2016).
Serikali ya Jamuhuri ya
Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia,
Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Wadau wake imechukua hatua za
makusudi na za haraka katika kukabiliana na Maambukizi ya Virusi vya
UKIMWI na UKIMWI. Serikali imefanikiwa kuanzisha na kutekeleza mipango
mbalimbali ya kuzuia maambukizi mapya kwa kutoa huduma za kinga, tiba na
matunzo kwa walioambukizwa VVU katika ngazi ya vituo vya huduma za afya
na ngazi ya jamii. Mikakati yote hii imelenga kuboresha afya kwa
kupunguza maambukizi mapya ya VVU na kutokomeza kabisa UKIMWI.
Mbali na Mipango mikakati na
mbinu madhubuti ambazo zimetekelezwa bado takwimu zinaonesha kuwa
kiwango cha maambukizi miongoni mwa makundi maalum na yale yaliyo katika
hatari zaidi ya kuambukizwa VVU yapo juu kulinganisha na kiwango
kilichopo kwa jamii kwa ujumla.


No comments:
Post a Comment