KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 26, 2016

WAZIRI WA AFYA ATOA TAMKO JUU YA VIASHIRIA NA MAABUKIZI YA UGONJWA WA UKIMWI NA MARALIA KWA TAKWIMU ZA 2011-2012

1
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na WatotoMh. Ummy Mwalimu akizungumza na waandishi wa habari wakati alipokuwa akitoa tamko la serikali kuhusu Takwimu za viashiria vya Ukimwi na Maralia mwaka 2011-2012 na kiwango cha maambukizi ya Ukimwi (VVU) kushoto kwake ni Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Mohammed Bakari Kambi.
……………………………………………………………………
Kwa mujibu wa Takwimu za Viashiria vya UKIMWI na Malaria za mwaka 2011-2012, kiwango cha maambukizi ya Virusi vya UKIMWI (VVU) nchini kinakadiriwa kuwa ni asilimia 5.1 miongoni mwa watu wazima wenye umri kati ya miaka 15 – 49. Takwimu hizi zinaashiria kwamba, kwa kila watanzania 1000, watu 51 miongoni mwao wanaoishi na maambukizi ya VVU. Inakadiriwa kuwa, kuna watu 1,400,000 wanaishi na VVU nchini Tanzania ambapo, watu 839,574 wanapatiwa tiba ya dawa za kupunguza makali ya VVU zinazotolewa katika vituo 4,000 vilikuwa vinatoa huduma hiyo nchi nzima hadi kufikia mwezi Juni mwaka huu (2016).
Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa kushirikiana na Wadau wake imechukua hatua za makusudi na za haraka katika kukabiliana na Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Serikali imefanikiwa kuanzisha na kutekeleza mipango mbalimbali ya kuzuia maambukizi mapya kwa kutoa huduma za kinga, tiba na matunzo kwa walioambukizwa VVU katika ngazi ya vituo vya huduma za afya na ngazi ya jamii. Mikakati yote hii imelenga kuboresha afya kwa kupunguza maambukizi mapya ya VVU na kutokomeza kabisa UKIMWI.  
Mbali na Mipango mikakati na mbinu madhubuti ambazo zimetekelezwa bado takwimu zinaonesha kuwa kiwango cha maambukizi miongoni mwa makundi maalum na yale yaliyo katika hatari zaidi ya kuambukizwa VVU yapo juu kulinganisha na kiwango kilichopo kwa jamii kwa ujumla.

No comments:

Post a Comment