KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 17, 2017

SILAHA MBALIMBALI ZAKAMATWA PORI LA VIKINDU

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es salaam, limekamata silaha tano na risasi 12, katika pori la vikindu, zikiwa zimetelekezwa kufuatia operesheni maalumu ya siku saba.

Operesheni hiyo ililenga kukamata magari ya wizi, majambazi, wauzaji wa dawa za kulevya, wauza gongo na makosa ya usalama barabarani.

Mbali na hilo, operesheni hiyo imefanikiwa kukusanya sh. 215,090,000,kutokana na makosa mbalimbali ya usalama barabarani kuanzia januari 13 mpaka 15, mwaka huu.

Hayo yamesemwa na Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es salaam, Simon Sirro.Amesema kuwa wamefanya operesheni hiyo katika pori la vikindu, Mkoani Pwani kufuatia ongezeko la matukio ya uhalifu katika maeneo mbalimbali ya Dar es salaam.

Aidha, Sirro amesema kuwa watuhumiwa 362, walikamatwa na makosa mbalimbali na kuongeza kuwa wamekamata silaha aina ya SMG moja, shortgun mbili na bastola mbili.

Hata hivyo, Sirro amesema kuwa katika operesheni hiyo imebainisha maeneo yaliyokithiri kwa matukio ya uhalifu ni Kigogo Freshi na Yombo Vituka

No comments:

Post a Comment