KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 17, 2017

WAZIRI NAPE AWAJIBU WALIOBEZA DIAMOND KUKABIDHIWA BENDERA YA TAIFA

Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Tanzania Nape Nnauye sio kwamba hakuona maoni ya Watanzania kwenye mitandao ya kijamii baada ya yeye kumkabidhi bendera mwimbaji wa bongofleva Diamond Platnumz kwenda Gabon kwenye michuano ya Afrika.

Waziri Nape ameziona comments za Watanzania na yeye amewajibu baada ya Diamond kuhudhuria kwenda kutumbuiza kwenye mashindano hayo ya soka Afrika yanayofanyika Gabon ambapo Nape baada ya kuona imekua gumzo mitandaoni yeye kumpa Diamond bendera.

Kupitia Twitter  yake Waziri Nape alichukua picha ya Diamond akiwa na wengine wa Afrika walioziwakilisha nchi zao kwenye mashindano yao wakiwa na bendera na kuandika "Ulizeni tena kwanini nilimkabidhi bendera Diamond"
 
==>Kwa sababu mjadala umekua mrefu sana kupitia twitter,baada ya post ya Waziri Nape kwenye watu walioandika tena ni Mbunge Ridhiwani Kikwete ambaye ameandika: Nafikiri Waziri amepanik kutokana na mashambulizi lkn ukweli ni kuwa tunahitaji kushiriki afcon 2019



No comments:

Post a Comment