KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

February 13, 2017

MAJINA YA WAFANYABIASHARA YA DAWA ZA KULEVYA YAKABIDHIWA KWA KAMISHNA WA KUPAMBANA NA DAWA ZA KULEVYA

Shekh  wa Mkoa wa Dar es salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya Amani Alhadi Mussa akizungumza na watendaji mbalimbali wa vyombo vya ulinzi na usalama mkoa wa Dar es salaam pamoja na viongozi mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi, Wenyeviti wa serikali za mitaa na madiwani pamoja na vijana mbalimbali waliokuwa wanatumia dawa za kulevya katika mkutano wa taarifa ya maendeleo ya Kampeni ya kupiga vita dhidi ya madawa ya kulevya.
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam amekabidhi majina mengine 97 ya awamu ya tatu kwa Bw. Rogers William sianga kuwa kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya  ili yaanze kushughulikiwa amesema awamu hii itaitikisa nchi kwani wameanzia toka awamu ya tatu iliyoongozwa na Rais Mstaafu Ali Hassan Mwinyi, ya nne Rais Mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete  na hii ya Tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli.
Mchungaji Geoge Fupe wa KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani akizungumza katika mkutano huo
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akizungumza jambo na  Bw. Rogers William sianga kuwa kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya katika mkutano wa kutoa tathmini ya kampeni ya kutokomeza madawa ya kulevya Kamishna katika mkoa wa Dar es salaam.
Mkuu wa  mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda akiwa pamoja na viongozi wengine wakiwa katika mkutano huo.
Kamanda wa Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamishna Saimon Sirro akizungumzo wakati akitoa taarifa ya kampeni hiyo leo.

No comments:

Post a Comment