Na Mwamvua Mwinyi,Rufiji
MKUU wa mkoa wa Pwani,
mhandisi Evarist Ndikilo, amehimiza kupanda mazao yanayostahimili ukame
na kukomaa haraka ikiwa ni sanjali na muhogo, mtama, viazi vitamu na
kunde.
Amesema wakati mvua zikiendelea kunyesha haina budi watu
wakalima mazao hayo ili kujiepusha na baa la njaa ambalo huwa
likijitokeza katika baadhi ya maeneo.
Mhandisi Ndikilo, ameeleza hayo katika ziara yake aliyoianza
mkoani hapo kutembelea wilaya sita kujionea hali ya mazao mbalimbali ya
Kilimo na kuhamasisha Kilimo.
“Kipindi hiki hali ya hewa sio nzuri sana na utabiri wa hali ya
hewa ulitabiri hakutokuwa na mvua za vuli za kutosha na ilitokea”
“Na za masika zinavyoonekana zitakuwa chini ya wastani hivyo
tusipojipanga na Kilimo na kutokuwa waangalifu tutatumbukia kwenye njaa
“alisema mhandisi Ndikilo.
Mhandisi Ndikilo alisisitiza kulima mazao yanayostahimili ukame ili kuwa na chakula cha kutosha.
Hata hivyo, aliambiwa na wakazi wa Mbwara wilayani Rufiji kuwa
mihogo wanalima lakini tatizo ni wanyama kama ngedere, nguruwe ambao
wanaharibu na kula mazao.
Mkuu huyo wa mkoa wa
Pwani alisema, watumie maafisa maliasili wilaya kwa kuandika barua
maalum kwa Mkurugenzi wa halmashauri na wataalam watakwenda kutatua
tatizo hilo.
Mhandisi Ndikilo akiwa wilaya ya Rufiji, alikagua ghala jipya la Ikwiriri AMCOS ,kukagua mashamba ya mihogo kijiji cha Mbwara.
Pia alitembelea mradi wa ujenzi wa nyumba za walimu Mbwara
sekondari na kuzungumza na waandishi. Mhandisi Ndikilo ameendelea na
ziara yake wilaya ya Kibiti na march 22 atakuwa Mkuranga
|
March 21, 2017
RC PWANI AHIMIZA KILIMO ILI KUJIEPUSHA NA BAA LA NJAA
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment