Kikosi cha Timu ya Taifa ya
Tanzania Taifa Stars kilichocheza na timu ya taifa ya Botswana leo
kwenye uwanja wa Taifa kikiongozwa na mchezaji wa kulipwa anayechezea
timu ya Genk ya Ubelgiji Mbwana Samata.
Waziri wa Habri, Sanaa, Utamaduni
na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe akisalimiana na wachezaji wa timu ya
taifa ya Botswana kabla ya mchezo huo kwenye uwanja wa Taifa leo.
Waziri wa Habri, Sanaa, Utamaduni
na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe akisalimiana na wachezaji wa timu ya
taifa ya Tanzania Taifa Sytars kabla ya kuchezwa kwa mchezo huo kwenye
uwanja wa Taifa.
……………………………………………………………………………………
Mshambuliaji wa Kimataifa na pia
hucheza Ligi Kuu ya Ubelgiji Mbwana Ally Samatta ameisaidia Taifa Stars
kuibuka na ushindi wa magoli 2-0 dhidi ya Botswana huku yeye akifunga
magoli yote mawili mchezo wa kimataifa wa kirafiki uliochezwa kwenye
uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
Na ulikuwa mchezo wa kwanza Taifa Stars inacheza chini ya kocha
wake mpya, Salum Mayanga aliyerithi mikoba ya Charles Boniface Mkwasa
aliyeng’atuka Janauri.
Katika mchezo huo uliodhuhuriwa na Waziri mpya wa Habari,
Utamaduni Sanaa na Michezo, DK Harison Mwakyembe, ilimchukua dakika
mbili tu mshambuliaji huyo wa KRC Genk ya Ubelgiji kuwainua vitini
wapenzi wa soka wa Tanzania waliojitokeza kuangalia Mpira huo akimalizia
pasi ya beki Mohamed Hussein Tshabalala na kumtoka beki Kaone
Vanderwesthuizem kabla ya kumchambua kipa, Kabelo Dambe.
Baada ya bao hilo, Botswana
wakabadilisha aina ya uchezaji na kuacha kujilinda zaidi na badala yake
kuanza kupeleka mashambulizi langoni mwa Stars.
Hali hiyo iliitia misukosuko kidogo ngome ya Taifa Stars,
lakini siofa zimuendee kipa Aishi Salum Manula aliyeokoa hatari zote.
Kipindi cha pili, mchezo uliendelea kuwa wa kushambuliana kwa zamu, ingawa Stars ndiyo wal8oendelea kung’ara zaidi uwanjani.
Wafungaji hodari katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara,
Shiza Kichuya wa Simba SC na Simon Msuva wa Yanga haikuwa bahati yao
leo, kwani walipoteza nafasi kadhaa nzuri za kufunga.
Winga Farid Mussa wa Tenerife ya Hispania alimkatia pasi nzuri
Nahodha Samatta na wakati analielekea lango la Botswana akaangushwa na
Thero Setsile nje kidogo ya boksi.
Samatta akaenda mwenyewe kupiga shuti la mpira wa adhabu kiufundi na kuifungia bao la pili Taifa Stars dakika ya 87.
Kikosi cha Tanzania kilikuwa: Aishi Manula, Shomari Kapombe,
Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Erasto Nyoni, Abdi Banda, Himid Mao/Jonas
Mkude, Simon Msuva/Said Ndemla, Frank Domayo/Muzamil Yassin, Mbwana
Samatta, Ibrahim Hajib na Shiza Kichuya/Farid Mussa.
Botswana: Kabelo Dambe, Tapiwa Gadibolae, Kaone
Vanderwesthuizem, Lesenya Ramoraka, Lesego Galenamotlhale, Ofentse
Nato, Lebogang Ditsele, Omaaatla Kebatho, Mosha Gaolaolwe, Thacng
Sesenyi na Mogakolod Ngele
No comments:
Post a Comment