KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

March 11, 2017

YANGA YABANWA MBAVU NA ZANACO FC LIGI YA MABINGWA AFRIKA

Yanga-300x200

Wawakilishi wa Tanzania katika Michuano ya Klabu bingwa ya Afrika Yanga  wamejiweka katika hali mbaya ya kusonga mbele baada ya kulazimishwa sare ya kufungana bao 1-1 na Zanaco ya Zambia katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 32 bora katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Matokeo yanamaanisha Yanga watahitaji ushindi wa ugenini katika mchezo wa marudiano nchini Zambia ili kuingia hatua ya makundi ya michuano hiyo.
Simon Msuva aliifungia Yanga dakika ya 39 akimalizia pasi nzuri ya Mzambia Justine Zulu hadi mapumziko wenyeji walikuwa mbele kwa bao 1-0. Kipindi cha pili Zanaco walikuja na mbinu  mapya na kufanikiwa kuziba mianya ya Yanga kupasiana pasi hivyo kuweza kutawaala eneo la kiungo cha kati na kuwafanya vijana wa Lwandamina kushindwa kutawala katikati.
Mshambuliaji wa kulipwa kutoka nchini Ghana Attram Kwame aliisawazishia Zanaco dakika ya 78 kutokana na Mpira uliochezwa kwenye eneo la 18 la Yanga na kumkuta mfungaji akiwa kwenye nafasi ya kufunga huku akiwa peke yake na kumchambua mlinda mlango wa Yanga Dida.
Hadi Mpira unamalizika Yanga wameweza kugawana pointi na Wazambia hao na kujiweka katika wakati Mgumu wa kutinga kwenye hatua ya makundi huku wakihitaji ushindi zaidi katika mchezo wa marudiano utakaochezwa Machi 17 au 18 mwaka huu mjini Lusaka Zambia
VIKOSI: Deogratius Munishi ‘Dida’, Hassan Kessy, Mwinyi Hajji, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Vincent Bossou, Kevin Yondan, Simon Msuva, Justin Zulu, Donald Ngoma/Emmanuel Martin dk58, Thabani kamusoko/Juma Mahadhi dk60 na Obrey Chirwa.
Zanaco; Racha Kola, Ziyo Kola, Zimiseleni Moyo, Chongo Chirwa, Saith Sakala/Kennedy Musonda dk69, Taonga Mbwemya, Richard Kasonde, Attram Kwame, Augustine Mulenga, Ernest Mbewe na George Chilufya

No comments:

Post a Comment