Makamu wa Rais wa zamani wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Athumani Nyamlani amejitoa
kwenye kinyang’anyiro cha kuwania urais wa shirikisho hilo unaotarajiwa
kufanyika Agosti 12, mwaka huu.
Nyamlani aliwasilisha barua TFF
leo Jumapili Juni 25, mwaka huu ikiwa ni siku moja tu tangu Kamati ya
Uchaguzi ipitishe jina lake kuwa miongoni mwa wagombea 10 wanaowania
nafasi hiyo ya urais. Sababu aliyoeleza ni masuala binafsi.
Kwa msingi huo, wagombea
wanaobaki kwenye kinyang’anyiro na kuhitajika kufika kwenye usaili
kuanzia Juni 29, mwaka huu ni tisa wakiongozwa na Rais wa sasa, Jamal
Malinzi anayetetea nafasi.
Mbali ya Malinzi wengine
wanaowania nafasi hiyo ni Imani Madega, Wallace Karia, Fredrick Masolwa,
Fredrick Mwakalebela, John Kijumbe, Shija Richard, Ally Mayay na
Emmanuel Kimbe.
Waliojitokeza kuwania Makamu wa
Rais na kurejesha fomu wako Mulamu Ng’hambi, Michael Wambura, Geofrey
Nyange, Mtemi Ramadhani, Robert Selasela na Stephen Mwakibolwa.
Mbali ya nafasi za urais na
makamu rais, Abdallah Mussa – aliyekuwa akiwania nafasi ya kugombea
ujumbe wa Kamati ya Utendaji TFF kutoka Kanda Na. 1 (Mikoa ya Kagera na
Geita) aliondolewa kwa sababu ya kutoambatanisha kivuli cha cheti ya
elimu ya sekondari.
Hivyo wagombea wa nafasi za Wajumbe wa Kamati ya Utendaji kwa kufuata Kanda 13 ni kama ifuatavyo:
No comments:
Post a Comment