IDARA
ya Uhamiaji Mkoani Tanga imewakamata wahamiaji haramu 45 kutoka nchini
Ethiopia katika Kijiji cha Horohoro wilayani Mkinga mkoani Tanga kwa
kosa la kuingia nchini kinyume cha sheria wakiwa shambani kwa wananchi
wanakula mahindi kabla ya kutiwa nguvuni.
Licha ya kukamatwa kwa wahamiaji haramu hao lakini pia idara hiyo inamshikilia raia mmoja kutoka
nchini Kenya ambaye ndio alikuwa akiwaongoza wahamiaji haramu hapa.
Akizungumza na waandishi wa habari,Afisa Uhamiaji Mkoa wa Tanga, Crispin Ngonyani alisema wahamiaji
haramu hao walikamatwa June 18 mwaka huu katika kijiji hicho baada kupata taarifa kutoka
kwa wasamaria wema wa eneo hilo.
Alisema wahamiaji haramu hao walikamatwa wakiwa porini katika jiji hicho wakati wakisafiri kuelekea nchini Afrika Kusini ambapo waligunduliwa na wananchi baada ya kufika mashambani mwao wakawakuta wanakula mahindi ndio walipotoa taarifa kwa askari wa Polisi wa Horohoro na hivyo wakaenda kuwakamata.
Licha ya kukamatwa kwa wahamiaji haramu hao lakini pia idara hiyo inamshikilia raia mmoja kutoka
nchini Kenya ambaye ndio alikuwa akiwaongoza wahamiaji haramu hapa.
Akizungumza na waandishi wa habari,Afisa Uhamiaji Mkoa wa Tanga, Crispin Ngonyani alisema wahamiaji
haramu hao walikamatwa June 18 mwaka huu katika kijiji hicho baada kupata taarifa kutoka
kwa wasamaria wema wa eneo hilo.
Alisema wahamiaji haramu hao walikamatwa wakiwa porini katika jiji hicho wakati wakisafiri kuelekea nchini Afrika Kusini ambapo waligunduliwa na wananchi baada ya kufika mashambani mwao wakawakuta wanakula mahindi ndio walipotoa taarifa kwa askari wa Polisi wa Horohoro na hivyo wakaenda kuwakamata.
No comments:
Post a Comment