Mbunge
wa jimbo Ubungo,(CHADEMA) Saed Kubenea ameitwa polisi na kutakiwa
kuripoti leo tarehe 20/7/ 2017 kutoa maelezo kituo cha polisi kufuatia
malalamiko aliyotoa Profesa Lipumba Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na
Msajili wa Vyama vya Siasa nchini.
Mbunge
wa Ubungo Mh Saed Kubenea wiki iliyopita alifanya mkutano na vyombo vya
habari kama Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani akiwa pamoja na baadhi ya
viongozi wa CUF iliyochini ya uongozi wa Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif
na kutangaza oparesheni ya kumuondoa Profesa Lipumba katika ofisi za
chama cha CUF Buguruni.
Baada
ya Kubenea kutangaza oparesheni hiyo siku mbili mbele aliibuka Profesa
Lipumba na kwenda kituo cha polisi kutoa malalamiko juu ya kile
alichokisikia kutoka kwa kiongozi huyo na oparesheni hiyo aliyotangaza.
"Ni
kweli Kubenea ameitwa na kuitwa kwake kumekuja baada ya wiki iliyopita
kufanya mkutano na waandishi wa habari kama Makamu Mwenyekiti wa Kanda
ya Pwani akiwa pamoja na viongozi wa CUF inayoongozwa na Mwenyekiti wa
Kamati ya Uongozi, Julius Mtatiro na Katibu Mkuu Maalim Seif na
kutangaza operesheni inayoitwa 'Operesheni Ondoa Msaliti Buguruni (OMB).
Operesheni hiyo itaendeshwa kwa ushirikiano wa vyama vinavyounda UKAWA" ilisema taarifa ya CHADEMA
No comments:
Post a Comment