Wakicheza bila ya
mshambuliaji wao hatari Neymr amabye amehamia PSG pamoja na Luis Suarez
aliye na majeruhi timu ya Barcelona imeanza vyema katika kusaka taji la
Ligi Kuu ya Hispania kwa kupata ushindi wa magoli 2-0 katika mechi yake
ya La Liga dhidi ya Real Betis.
Wakicheza kwa
kujiamini licha ya kufungwa na mahasimu wao wakubwa Real Madrid katika
mchezo wa Ngao ya Hisani walipata magoli yao kupitia kwa Alin Tosco
aliyejifunga dakika ya 36 huku beki Sergio Roberto akipingilia msumari
wa pili dakika ya 39.
Kipindi cha pili
kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko hata hivyo mabadiliko hayo
hayakuweza kuwasaidia Real Betis hadi dakika 90 Barcelona wameibuka na
ushindi wa jumla ya magoli 2-0 na pointi tatu muhimu.
Katika Uwanja wa Camp
Nou, kulikuwa na ulinzi wa ziada kutokana na shambulio la kigaidi
lililotokea siku tatu zilizopita na kusababisha vifo vya watu 14.
No comments:
Post a Comment