KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

September 26, 2017

MBEYA CITY YAPATA KOCHA MPYA KUTOKA BURUNDI

22007404_493126874400429_3872412639073796972_n
Klabu ya Mbeya City imefikia makubaliano na Kocha Nsanzurwimo Ramadhani kuwa Kocha Mkuu kwa mkataba wa awali wa Msimu mmoja wa ligi kuu ya Vodacom inayoendelea.
Kocha Ramadhan ni raia wa Burundi na anatarajiwa kujiunga na timu hiyo huko kanda ya ziwa inakoendelea na michezo yake ya ligi kuu.
Kocha Ramadhani amewahi kuwa kocha kwa nyakati tofauti katika vilabu mbalimbali nchini Burundi, Rwanda, Botswana, Malawi, Uganda, na Afrika ya Kusini, pia amewahi kuwa mshauri wa ufundi katika timu ya taifa ya Burundi na kocha msaidizi/kocha mkuu wa muda(caretaker) kwa timu ya taifa ya Malawi.
Imetolewa na
Shah Mjanja Afisa Habari MCCFC
0717282217

No comments:

Post a Comment