Makamu
Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Chadema (BAVICHA), Patrick Ole Sosopi
amesema kwamba kuondoka kwa Mwenyekiti wa baraza hilo Patrobas Katambi
ndani ya Chama hicho hakijawateteresha na kudai kwamba Katambi hakuwa
mkubwa kuliko Chama chao.
Akizungumza
jana muda mfupi baada ya Mwenenyekiti wa Baraza hilo kuhamia CCM, Ole
Sosopi alisema kwamba Patrobasi hakuwa Bavicha kwani aliingia ndani ya
chama hicho akiwa hana umaarufu hivyo kuondoka kwake kusiwavunje moyo
vijana vingine na kusisitiza kwamba bado baraza hilo la vijana lipo
imara.
"Patrobas siyo Bavicha, ila yeye alikuwa sehemu ya Bavicha. Bavicha ipo imara na hii ni taasisi.
"Na
Patrobasi kuondoka Chadema siyo jambo geni, ni jambo la kawaida kama
jinsi viongozi wengine wavyotoka chama kimoja kwenda kikingine.
"Tunamtakia
kila la kheri huko alipokwenda. Vijana wetu waendelee kuiwa busy
kufanya kampeni kwa ajili ya uchaguzi na wasihangaike na habari za
Patrobas". Alisema Ole Sosopi na kuongeza;
"Ndani
ya Chadema hakuna mtu maarufu isipokuwa Patrobas alipata umaarufu
alipokuwa ndani ya Chama na ameondoka, hivyo Chama kitaendelea kuwa
imara siyo kwa ajili ya mtu mmoja. Kupitia uchaguzi huu mdogo tunapaswa
kutuma meseji kwa CCM na yeye Katambi hivyo vijana msihamishwe na hili
jambo mkaacha kuendeleza kampeni".
Aidha
aliongeza kwamba kitendo cha Patrobas kuhamia CCM ni usaliti ambao
ameudhihirisha kwa watanzania na wanachama kuungana na watu au serikali
ambayo imeshindwa kumbaini nani aliyempiga risasi mwanasheria mwenzake
Tundu Lissu.
Aliongeza
kwamba kinachofanywa na CCM siyo siasa bali ni 'Project' inayofanyika
kushawishi watu waone kwamba CCM imebadilika lakini ukweli ni kwamba
"CCM ni ileile na madudu yake ni yaleyale kwa zaidi ya mika 50
nawashauri wafanye siasa zinazohgusa wananchi"
No comments:
Post a Comment