Lazaro Nyalandu
Mapema
leo taarifa kutoka ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambapo
hivi karibuni alihamia zilibainisha kuwa angeweza kuhutubia katika kampeni za
udiwani mkoani humo.
Akithibitisha
hilo Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema
amesema sababu ni kukosekana kwa ndege ya kuunganisha kutokea Dar es Salaam
kwenda Mtwara..
“Kumemsababishia
Nyalandu kushindwa kuhudhuria mkutano huo, kwani alikuwa Nairobi nchini
Kenya kumjulia hali Tundu Lissu,” amesema Mrema.
Mrema
amesema Nyalandu amefika Dar es Salaam na kukosa ndege ya kwenda Mtwara, hivyo
amewaomba radhi wananchi ambao walikuwa wanasubiria kumsikiliza Nyalandu na
kwamba wanaandaa kwa ajili ya siku nyingine kuweza kufanya hivyo.
"Tunaomba
radhi kwa hili ila tukio hilo tunaliandalia mahali pengine na wakati ukifika
tutakuwa pamoja naye," amesema Mrema.
No comments:
Post a Comment