Msanii
wa muziki wa kizazi kipya, Judith Wambura, maarufu "Lady Jay Dee"
ameendelea kuonyesha ukongwe wake katika sanaa hiyo baada ya jana
kutambulisha kibao chake kipya kiitwacho Anaweza.
Lady
Jay Dee au Komando ameutambulisha wimbo huo sambamba na kutoa video ili
kuwavuta karibu mashabiki wake ambao wanafahamu kiwango chake.
Lady
Jay Dee, alisema kuwa kibao hicho kitengenezwa na mtayarishaji Spicy
Judoka wa Nigeria huku video ikisimamiwa na Justin Compus Lutona wa
Afrika ya Kusini na lengo la kuchanganya wataalamu hao ni kuhakikisha
kazi yake inakuwa na hadhi ya kimataifa.
Alisema
kuwa baada ya kukamilisha kazi hiyo, anajiandaa kufanya onyesho la
muziki na tayari ameanza maandalizi kwa ajili ya kuwapa furaha mashabiki
wake.
Aliwataja
wasanii wengine ambao wanamuunga mkono kuwa ni Rutta Bushoke, Nikki
Mbishi na Judoka anayeimba muziki wa Hip Hop na kueleza kuwa nyota
wengine atawatangaza hapo baadaye.
“'Nimemiss'
jukwaa, nimemiss watu wangu, nimemiss ile kazi ya kusimama masaa kadhaa
na kuwasiliana na watu wanaounga mkono muziki wangu kwa miaka nenda,
rudi.
Nimeamua
sasa kuwa nitafanya haya matamasha mara kwa mara ili mwisho wa siku
muziki wangu uendelee kuishi miongoni mwa mashabiki wangu kwa sababu
tukisema ukweli ndio kitu ninachokipenda, muziki”, alisema Lady Jay Dee
ambaye ana albamu saba.
No comments:
Post a Comment