KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

March 28, 2015

JK ATOA MAAGIZO MAKALI,RIPOTI YA CAG

3jgghh
Rais Jakaya Kikwete amekabidhiwa Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka unaoishia Juni 2014 na kuagiza vyombo vya dola kuwabaini maofisa wote wa Serikali wanaohusishwa na matumizi mabaya ya fedha za umma, ili wachukuliwe hatua kali za kisheria.
Pia, Rais Kikwete ameagiza kuchukuliwa kwa hatua kali za kisheria kwa maofisa wote wa Serikali ambao wanahusika katika kulipa mishahara hewa kwa watumishi ambao wameacha kazi, wamefariki dunia au wamestaafu lakini wanaendelea kulipwa kupitia akaunti zao za benki.
Rais ametoa maagizo hayo jana baada ya kukabidhiwa ripoti hiyo na CAG Profesa Mussa Assad. Aliiomba ofisi hiyo kuisaidia Serikali kuboresha mfumo wa zabuni kwani Serikali inapoteza fedha nyingi kwa kupitia mchakato mrefu wa kupatikana kwa wazabuni wa kutoa vifaa na huduma kwa Serikali

No comments:

Post a Comment