KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 2, 2015

GWAJIMA AMGOMEA MAKONDA

makonda
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
MKUU wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda amemwandikia barua Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima akimtaka afike mbele ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya kwa mahojiano. Inaelezwa kuwa Makonda alimtumia Askofu Gwajima barua hiyo Machi 30 mwaka huu, akiwa amelazwa katika Hospitali ya TMJ. Hata hivyo, kiongozi huyo wa kiroho amegoma akisema hawezikwenda ofisini kwa mkuu huyo wa wilaya kwa mahojiano. Mmoja wa wasaidizi wa Askofu Gwajima aliliambia MTANZANIA jana kuwa hatua ya Makonda kumtumia barua haikumpendeza kiongozi huyo wa kanisa. “Makonda alikuja katika Hospitali ya TMJ na kudai amekuja kumwona Askofu Gwajima huku akiwa amebeba barua yake. Baada ya kumwuliza hali ya maendeleo ya afya yake alitoa barua na kumkabidhi jambo ambalo halikuwa jema. “Baada ya muda Askofu Gwajima alituita wasaidizi wake na kutueleza kuwa amepewa barua ya wito kwa DC, sasa tukajiuliza askofu anaumwa. Je, inakuaje aende tena katika mahojiano na mkuu wa wilaya? “Na kama ni hivyo nini kazi ya polisi maana wamemuhoji tangu siku ya kwanza baada ya kumkamata. Je, inakuaje tena Makonda alete barua ya kumtaka askofu akahojiwe tena mbele ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya mbele ya DC? “Hapa kuna mchezo unataka kufanywa na je, katika masuala haya ya usalama sijui kama huyo DC anajua wajibu wake. Mtu anahojiwa na polisi sasa inakuaje tena aitwe na DC ahojiwe na kamati ya ulinzi? Amesema hatokwenda,”CHANZO:MTANZANIA

No comments:

Post a Comment