KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 2, 2015

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI




                   SHIRIKISHO LA NGUMI TANZANIA

                             Yah:- Timu ya Taifa ya Ngumi 2015.



Hatimaye baada ya mchakato wa muda mrefu,  uliofanyika kwa umakini kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa hatimaye Shirikisho la Ngumi Tanzania (BFT) limepata wachezaji wa timu ya Taifa ya Ngumi 2015. Katika mashindano ya kimataifa  yaliyoshirikisha timu za taifa kutoka Uganda na Kenya, mashindano yaliyomalizika kwa mafanikio, Jumamosi ya tarehe 28.03.2015 uwanja wa Taifa wa ndani .

Mabondia waliochaguliwa kwa sasa taratibu za kuombewa ruhusa katika timu zao zinafanyika na taratibu hizo zitakapo kamilika watatakiwa kuanza mazoezi kabla ya tarehe 15.04.2015, kwa ajili ya kushiliki mashindano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa hasa mashindano  ya Michezo ya Afrika (All African Games) Septemba 4-19. Brazzaville Congo. Na mashindano ya Ubingwa wa Dunia (AIBA World Boxing Championships) Octoba 5-18 Doha Qatar.




Nakala kwenu kwa  Taarifa.


Makore Mashaga

Katibu Mkuu (BFT)

No comments:

Post a Comment