KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 14, 2016

HUDUMA HOSPITALI YA KOROGWE ZAMKERA KIGWANGALA


Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Hamisi Kigwangalla ametoa siku 60 kwa uongozi wa Hospitali ya Wilaya ya Korogwe, Magunga, kurekebisha miundombinu ya majitaka hususan wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji.
Alitoa  agizo hilo juzi baada ya kukagua shughuli za utaoji huduma, ikiwamo kushuhudia changamoto zinazowakabili.
Dk Kigwangalla alikumbana na changamoto ya uchakavu wa miundombinu ya majitaka, ambayo imekuwa kikwazo kwa utendaji wa watumishi na wagonjwa.
“Mfumo wa majitaka hapa hauko vizuri, ni hatari kwa afya zenu watumishi na wagonjwa, nawapeni siku 60 kuhakikisha mmefanyia marekebisho,” aliagiza.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dk Gwamaka Mwabulambo alimweleza Naibu Waziri huyo kwamba mwaka wa fedha wa 2016/17, zimetengwa Sh50 milioni kwa ajili ya ukarabati wa hospitali.
Mkuu wa Wilaya ya Korogwe, Hafsa Mtasiwa alisema agizo hilo limetolewa wakati mwafaka kwani litasaidia kunusuru milipuko ya magonjwa ya kuambukiza na aliahidi kulisimamia.

No comments:

Post a Comment