Vijana watano kutoka Tanzania ni miongoni mwa vijana 30 wanaoshiriki katika mafunzo ya wawezeshaji wa ujasiliamali unaozingatia mazingira yanayofanyika jijini Beja, nchini Ureno.
Mafunzo hao ambayo yanafanyika kwa muda wa siku saba yanalenga kuwajengea uwezo vijana hao kuendesha mafunzo kwa vijana wenzao katika nchi wanakotoka ili kusaidia kupunguza tatizo la ajira na uharibifu wa mazingira.
Nchi zinazoshiriki mafunzo hayo na majina ya taasisi zinazoshiriki kwenye mabano ni pamoja na wenyeji Ureno (Check In), Italia (Cesie), Argentina (Subiral Sur), Slovenia (Pina), Nepal (CNN) na Tanzania (TYCEN) ambapo kila nchini imewakilishwa na vijana watano chini ya mradi wa ujasiliamali wa kujali mazingira ‘Green Entrepreneurship’.
48
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja walipotembelea kiwanda cha kuchakata taka cha Resialentejo, wakiongozwa na Injinia wa kiwanda hicho Pedro Sobral.
50
Washiriki wakiwa katika picha ya pamoja walipotembelea Halimashauri ya Manispaa ya Jiji la Beja ambao walipokelewa na Sonia Calvario Mshauri wa Meya wa Manispaa hiyo.
Mkurugenzi wa TYCEN, Chris Ndalo kutoka Tanzania akitoa mada wakati mafunzo hayo.
Mmoja wa wawezeshaji katika mafunzo hayo, Olga  Kuczynska.