Wananchi
wamemkataa mwenyekiti wa kitongoji cha Mwanogi kijiji cha Bulima, Kata
ya Nyashimo wilayani Busega katika Mkoa wa Simiyu, wakimtuhumu kuweka
majina hewa katika mradi wa kuokoa kaya masikini unaosimamiwa na Mfuko
wa Maendeleo ya Jamii (Tasaf).
Mwenyekiti huyo wa kitongoji, Ester Ng’ombe anatuhumiwa pia kufanya kazi kwa ubaguzi wa vyama vya siasa.
Akizungumza
katika kikao, mwenyekiti wa kamati ya mipango na fedha ya kijiji cha
Bulima, Zablon Ntinika alisema wamefikia uamuzi wa kumsimamisha kazi
mwenyekiti huyo baada ya uchunguzi walioufanya kubaini majina matano
ambayo ni hewa yakipatiwa fedha.
Alisema
wamekuwa wakifuatilia kwa karibu mwenendo wa mwenyekiti huyo katika
utendaji wake wa kazi katika kitongoji hicho lakini wamebaini mengi.
Mwenyekiti huyo anayetuhumiwa, alipoulizwa kuhusu madai hayo, alisema kuwa yeye hayatambui bali ni siasa za chuki dhidi yake.
|
April 27, 2016
MWENYEKITI AWEKA MAJINA HEWA MRADI WA KUOKOA KAYA MASIKINI (TASAF )
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment