Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Misungwi mkoani Mwanza, Charles
Kitwanga (kulia) akizungumza na wananchi wa mji wa Misungwi kuhusu
masuala mbalimbali ya maendeleo ya jimbo hilo. Katika hotuba yake,
Kitwanga aliwaka wananchi hao kufanyakazi ili jimbo hilo lizidi kusonga
mbele. Pia Mbunge huyo alipiga marufuku uchezaji wa pool table wakati wa
kazi.
Mkazi wa Misungwi mjini, Songoro
Msafiri (kushoto) akimuuliza swali Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Misungwi mkoani Mwanza, Charles
Kitwanga (kulia aliyekaa), mara baada ya Mbunge huyo kumaliza kuzungumza
na wananchi hao na kuruhusu kuuliuzwa maswali mbalimbali yanayowakera
jimboni humo. Kitwanga aliwataka wananchi wa jimbo lake washirikiane ili
waliletee maendeleo jimbo lao.
Wananchi wa mjini Misungwi
wakimsikiliza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ambaye pia ni Mbunge wa
Jimbo la Misungwi mkoani Mwanza, Charles Kitwanga katika mkutano wa
hadhara uliofanyika mjini huo leo.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,
ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Misungwi mkoani Mwanza, Charles
Kitwanga akizungumza na mabalozi wa mashina wa CCM katika Ukumbi wa
Mikutano wa CCM Wilaya ya Misungwi. Kitwanga aliwashukuru mabalozi hao
kwa kumchagua na kuwaomba washirikiane zaidi ili kuliletea maendeleo
jimbo hilo. Picha zote na Felix Mwagara
No comments:
Post a Comment