Kama
ulipata nafasi ya kutizama mchezo wa Jumamosi kati ya Manchester United
na mabingwa watetezi wa kombe la EPL, Leicester City basi ni wazi
utakuwa unajua kuwa nahodha wa Man United, Wayne Rooney alianzia benchi
katika mchezo huo na kuingia kipindi cha pili dk. 83, mchezo ambao
ulimalizika kwa United kuibuka na ushindi wa goli 4-1.
Baada
ya mchezo kumalizika kocha wa Man United, Jose Mourinho alikutana na
maswali ya waandishi wa habari wakitaka kujua sababu ya Rooney kuanzia
benchi na Mourinho kusema sababu ya Rooney kuanzia benchi ni kutaka kuwa
na washambuliaji wawili wenye kasi na Mata kucheza nafasi yake hivyo
ikabidi Rooney kusubiri nje.
“Nahodha
wangu ni nahodha wangu tu, kama akiwa uwanjani au akiwa nyumbani ni
nahodha wangu, kwahiyo hilo sio tatizo. Katika kikosi chetu dhidi ya
Leicester tuliona suluhisho la kupambana nao ni kuwa na watu wawili
wenye kasi na Mata akacheza nafasi ambayo alitakiwa kucheza’
“Ni mchezaji wangu [Rooney], namwamini na ana furaha kama niliyonayo mimi muda huu na kwa timu,” alisema Mourinho.
No comments:
Post a Comment