KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 1, 2016

BODI YA TAIFA YA WAHASIBU NA WAKAGUZI WA HESABU (NBAA) YAFANYA MAHAFALI YA 38.

bod1
Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, Kulia, akiwahutubia wahitimu na jumuiya ya Bodi ya taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) (Hawako Pichani), wakati wa mahafali ya 38 ya Bodi hiyo, yaliyofanyika katika Kituo cha Bunju, nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam, kulia kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa NBAA, Bw. Pius Maneno na Mwenyekiti wa Kamati ya Elimu na Mafunzo wa Bodi hiyo, Bi. Anne Mbughuni.
bod2
Baadhi ya wahitimu wa taaluma ya juu ya uhasibu (CPA), wakiwa tayari kutunukiwa shahada zao na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, katika Mahafali ya 38 yaliyofanyika Katika kituo cha Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA) kilichopo Bunju, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
bod3
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, akimkabidhi cheti cha kufanya vizuri katika masomo ya taaluma ya juu ya uhasibu (CPA-T), Bi. Happiness Ngowi, wakati wa mahafali ya 38 ya Bodi hiyo yaliyofanyika Katika kituo cha Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu (NBAA), kilichopo Bunju, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
bod4
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, akitangaza kuwatunuku vyeti wahitimu wa taaluma ya juu ya uhasibu (CPA-T) waliofanya vizuri katika masomo yao, wakati wa mahafali ya 38 ya NBAA, yaliyofanyika Katika kituo cha Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu, kilichopo Bunju, nje kidogo ya  Jiji la Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment