Imefahamika
kuwa hewa ya ukaa ina asilimia kubwa katika gesijoto hivyo kusababisha
kumong’onyoka kwa ozoni na kupelekea kuongezeka kwa kiasi cha nyuzi joto
duniani na udororaji wa uchumi wa nchi
Hayo
yamebainishwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh.
Samia Suluhu Hassan katika uzinduzi wa kampani ya upandaji miti
ijulikanayo kama Mti Wangu katika mkao wa Dar e Salaam.
Mhe.
Suluhu alisema kwa kutambua athari za ongezeko la gesi joto hususani
hewa ya ukaa serikali kupitia mkoa wa Dar es Salaam imekuja na kampeni
ya kupanda miti ili kukabiliana na changamoto zitokanazo na mabadiliko
ya tabianchi.
Alisema
mkoa wa Dar es Salaam unazalisha tani 4500 kwa kila siku zitokanazo na
gesi za viwandani, vyombo vya usafiri, taka ngumu za viwandani na
majumbani ikiwa ni pamoja na uchomaji na utupaji taka hovyo hivyo
kupelekea serikali kwa kushirikiana na wadau kuanzisha kampeni hiyo
jijini Daar es Salaam.
Alizitaja
sababu nyingine za kampeni hiyo kuanzia Dar esSalaam ni pamoja na
makadirio ya ongezeko la wakazi kufikia 5,895,791 kwa mwaka 2017 hivyo
kusababisha kuongezeka kwa kiasi kikubwa cha uzalishaji wa hewa ya ukaa
kutokana na kuongezeka kwa mahitaji mbalimbali ya shughuli za binadamu
na viwanda kwa ujumla.
Alisema
tafiti mbalimbali zimeonyesha hewa ya ukaa inaongezeka jijini Dar es
Salaam kutokana na ongezeko la viwanda na idadi kubwa ya wakazi ambapo
kwa mwaka 2015 utafiti umeonyesha mkoa huo una viwanda 1854 kati ya
hivyo 480 ni vikubwa na 1374 ni vidogo.
“Nawaagiza
viongozi wa Serikali, taasisi binafsi, Asasi za kiraia na kila
mtanzania kwa ujumla kutunza mazingira na kupanda miti ni hatua moja
mbele katika kutunza mazingira yetu,” alisema Mh. Suluhu.
Akimkaribisha
mgeni rasmi katika uzinduzi wa kampeni hiyo, mkuu wa Mkoa wa Dar es
Salaam Mh. Paul Makonda alisema serikali imeweka chuma na minyororo ili
kulinda wananchi kuvuka eneo ambalo si sahihi na kuweza kuhatarisha
maisha yao kwa kugongwa na magari.
Alisema
wananchi wanapaswa kulinda vyuma hivyo kwa kuwa vinasaidia kufanya
mazingira yawe mazuri na kukinga miti na nyasi zilizopandwa kando ya
barabara hizo zisiharibiwe.
“Wale
wanaopita usiku na wale wanaoharibu, mtu yeyote akikamatwa ameiba chuma
kimoja faini yake ni kununua vyuma kumi na kuchukulia hatua kwa mujibu
wa sheria”.
No comments:
Post a Comment