KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 1, 2016

LIPUMBA ADAIWA KUANZA TIMUA TIMUA CUF


Ikiwa imepita siku moja tangu vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kutangaza kutomtambua Profesa Ibrahim Lipumba kuwa mwenyekiti halali wa Chama cha Wananchi (CUF).
Mapema asubuhi jana wakati kikao cha Ukawa kinaendelea, Lipumba alitengua uteuzi wa baadhi ya wakurugenzi na manaibu wakurugenzi aliodai kuwa aliwateua kwa mujibu wa katiba ya chama hicho.
Na kudai kwamba, kwa kuwa yeye ni mwenyekiti ana mamlaka ya kutengua teuzi alizofanya.
Wakurugenzi aliodai kutengua teuzi zake ni Ismail Jusa Raju ambaye ni Mkurugenzi wa Mambo ya Nje pamoja na Naibu wake Abdallah Mtolea. Mwengine ni Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi, Shaweji Mketo.
Wengine ni Kuruthumu Mchuchuri ambaye ni Mkurugenzi wa Haki za Binadamu na Sheria pamoja na Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama Mustafa Wandwi.
Hata hivyo, Modewjiblog.com iliwatafuta baadhi ya wakurugenzi waliodaiwa kuvuliwa wadhifa na Lipumba na kubahatika kuzungumza na Kuruthumu Mchuchuri. Mchuchuri ameuambia mtandao wa huu kuwa Lipumba hana mamlaka ya kutengua ukurugenzi wake.
Ameeleza kwamba, katiba ya CUF inasema kuwa, ili mkurugenzi mpya aidhinishwe na au aliyekuwepo atenguliwe wadhifa wake, inabidi Baraza Kuu la Uongozi Taifa la CUF lithibitishe uteuzi mpya au utenguzi wa mkurugenzi aliyepo.
Amesema, Lipumba hatofanikiwa kuteua wakurugenzi wapya kutokana kwamba hana baraza halali litakalothibitisha uteuzi wa atakaye mteua na utenguzi wake.
“Lipumba hana baraza kuu la kunitengua na au kuthibitisha mkurugenzi yeyote atakayemteua. Kwanza wajumbe halali wa baraza hilo zaidi ya 40 wamepiga kura ya kumtoa katika chama,” amesema Mchuchuri.
Ameongeza kuwa “Lipumba amestaafu na analitambua hilo na ndiyo maana awali kila akiandika barua ya kuhitaji lolote kutoka katika chama anajitambulisha kama mwenyekiti mstaafu. Kwa ufupi siasa kwa upande wake imemkalia vibaya hana jinsi,” amesema.
Modewjiblog.com haikuishia hapo, ilimtafuta Mketo kwa njia ya simu kwa ajili ya mahojiano zaidi lakini hakupatikana MO BLOG

No comments:

Post a Comment