KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

April 12, 2018

SPIKA NDUGAI AFANYA MABADILIKO UTARATIBU WA KUINGIA BUNGENI

Spika wa Bunge, Job Ndugai amelitangazia bunge leo kuhusu mabadiliko ya utaratibu  wa kuingia bungeni.

Akifungua kikao cha bunge cha leo Aprili 12, Ndugai amesema  utaratibu wa kuingia bungeni utabadilika ambapo  kuanzia sasa Spika, Naibu Spika na wenyeviti wa Bunge hawatatumia mlango mkuu kuingia ukumbi wa bunge,  bali mlango wa nyuma ila kwa matukio maalum.

“Utaratibu kama huo unatumika pia katika nchi nyingine kama India na Uingereza,nia ni kufanya maboresho kama mabunge yaliyoendelea,” amesema

Spika Ndugai amesema ingawa haimo kwenye kanuni, lakini mabadiliko hayo yanafanyika ili kuendana na nchi nyingine zilizoendelea.

No comments:

Post a Comment