Spika wa Bunge, Job Ndugai amelitangazia bunge leo kuhusu mabadiliko ya utaratibu wa kuingia bungeni.
Akifungua
kikao cha bunge cha leo Aprili 12, Ndugai amesema utaratibu wa kuingia
bungeni utabadilika ambapo kuanzia sasa Spika, Naibu Spika na
wenyeviti wa Bunge hawatatumia mlango mkuu kuingia ukumbi wa bunge,
bali mlango wa nyuma ila kwa matukio maalum.
“Utaratibu
kama huo unatumika pia katika nchi nyingine kama India na Uingereza,nia
ni kufanya maboresho kama mabunge yaliyoendelea,” amesema
Spika Ndugai amesema ingawa haimo kwenye kanuni, lakini mabadiliko hayo yanafanyika ili kuendana na nchi nyingine zilizoendelea.
No comments:
Post a Comment