KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

September 23, 2014

CHADEDEMA YADAI KUFANYA MAANDAMANO, POLISI YASEMA THUBUTU!

Kamishna na Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi,Paul Chagonja.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiOoxU1GE7r9jhZJpOSCnzv8weK-SSfqWIgFLBbfQLAUdsD53lviE8_O_nkdM9PoS_hjSnDlrjOt5uvnYbYlsPuURy_VvikHCy7PZ1CD88PiWwNz4P8M61HyfllvQEvN7WpIMbDG0zHH6I/s1600/2.JPG
Mkurugenzi wa Oganaizesheni,Mafunzo na Usimamizi wa Kanda wa CHADEMA,Benson Kigaila akionyesha barua za maombi ya kufanya maandamano katika maeneo mbalimbali. (Picha ya Maktaba)                       



Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kimedai kufanya maandamano katika maeneo kadhaa ya nchi na kudai kuwa maandamano hayo yataendelea leo katika maeneo mengine. 

Maandamano hayo yanalengo la kupinga Bunge Maalum la Katiba linaloendelea mjini Dodoma.
Mkurugenzi wa Oganaizesheni ya Mafunzo na Usimamizi wa Kanda,Benson Kigaila,aliiambia Radio One leo asubuhi kuwa maandamano hayo yamefanyika katika maeneo ya Songea,Mbinga,Kyela,Chunya,Mbalali,Simiyu,Meatu na Shinyanga.

Akadai kuwa wao wataendelea kuandamana na kwamba si lazima waombe kibali Polisi, akaongeza kusema wao wanawajibu wa kutoa taarifa Polisi tu.
Naye Kamishna wa Operesheni na Mafunzo wa Jeshi la Polisi, Paul Chagoja akiongea na Radio hiyo alikanusha na kusema hakuna maandamano yoyote yaliyofanyika.
Akawasihi wananchi kuendelea na shughuli zao za kila siku na kutojiingiza kwenye maandamano hayo ambayo alisema si halali.

        

No comments:

Post a Comment