Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia Mhe.Prof.Makame Mbarawa,akizungumza na Waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati wa utiaji saini mkataba wa Utendaji baina yake na Wenyeviti wa Bodi na Taasisi zilizo chini ya Wizara kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu ya taasisi zao kwa mwaka wa fedha 2014/14 |
Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa wote,Prof.John Mkoma, akiweka saini mkataba wa utendaji baina yake na Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia,Mhe.Prof.Makame Mbarawa kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu ya taasisi kwa mwaka wa fedha 2014/15 |
Waziri wa Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia Mhe.Prof.Makame Mbarawa,akipeana mkono na Prof.Mkoma baada ya kuwekeana saini mkataba
Waziri wa
Mawasiliano,Sayansi na Teknolojia Mhe.Prof.Makame Mbarawa,ameongoza zoezi la utiaji
saini Mkataba wa Utendaji baina yake na wenyeviti wa Bodi za Taasisi zilizo
chini ya Wizara kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu ya taasisi zao kwa mwaka
wa fedha 2014/15.
Lengo la
Mhe.Waziri la kuwekeana Mkataba wa Utendaji,na Wenyeviti wa Bodi ni kufuatilia
kwa karibu utekelezaji wa majukumu wa Bodi hizo ili kuleta ufanisi na tija
kwenye sekta ya TEHAMA , Sayansi na Teknolojia ili iweze kuendelea kuchangia ukuaji
wa uchumi na mchango wa sekta kwenye pato la taifa.
Aidha
Mhe.Mbarawa alisema mapitio ya utekelezaji wa mkataba huo yatafanyika kila
baada ya mizezi mitatu ili kufuatilia namna unavyotekelezwa na kubaini
changamoto zinazowakabili wenyeviti na Bodi za taasisi zilizo chini ya Wizara kabla
ya mwisho wa mwaka wa fedha wa 2014/15.
Taasisi zilizo chini ya Wizara ni pamoja
na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania,Tume
ya Taifa ya sayansi na teknolojia,Kampuni ya Simu Tanzania, Shirika la Posta Tanzania,
Taasisi ya Tayansi na Teknolojia,Chuo Kikuu Cha Sayansi na Teknolojia Mbeya,Taasisi
ya sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela,Tume ya Nguvu za Atomiki Tanzania na
Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote.
|
No comments:
Post a Comment