KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 27, 2014

CHANZO CHA MAJI IKORONGO MPANDA

unnamed3
Mhandisi Happiness Magalula, Naibu Katibu Mtendaji, anayesimamia Klasta ya Miundombinu na Huduma (mwenye sweta la blue), akitaka ufafanuzi wa miundombinu ya kuwezesha maji kuwafikia wananchi kutoka katika chanzo hicho. 

Na Mwandishi wetu, Katavi

Bomba la inchi kumi limetandazwa kutoka kwenye chanzo hicho mpaka mjini ambako kuna tanki kubwa la maji yanayosambazwa katika mji wa Mpanda na vitongoji vyake  

Chanzo cha maji cha chemichemi ya Ikorongo ambacho ni cha asili kipo kilometa 13.2 kutoka Mpanda Mjini, Mkoani Katavi. 

Chanzo hiki cha maji kinazungukwa na miti na uoto wa asili unaolinda maji hayo yawe safi na salama kwa matumizi ya binadamu.

Mhandisi wa Maji wa Mkoa wa Katavi, Magdalena Mkeremi, anasema chanzo hiki cha maji ni chemichemi yenye maji masafi yasiyokauka hata wakati wa kiangazi.

Chanzo hiki kina uwezo wa kuzalisha zaidi ya lita milioni sita kwa siku.

Mradi wa maji wa Mji wa Mpanda ni wa gharama nafuu kwa sababu hautumii pampu ya aina yoyote, bali maji husambazwa kwa njia ya mserereko (gravity).

Vile vile  maji kutoka kwenye tanki hilo na kwenda mjini na katika mitaa au vijiji pia hutumia mserereko, hivyo kurahisisha gharama zake.

Mradi huo wa maji wa vijiji kumi au mitaa kumi ya mji wa Mpanda unagharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Dunia chini ya mfumo wa Matokeo Makubwa Sasa.

“Maji yalikuwa tatizo kubwa hapa kwetu lakini ujio wa mradi huu umerahisisha upatikanaji wa maji mjini na kwenye mitaa ya mji wa Mpanda,” anasema Mhandisi.

Tayari vimejengwa vituo vya kuchotea maji 41 katika mitaa kumi na watu binafsi wapatao 300 wameunganishiwa maji kupitia chanzo hicho cha maji.

Amesema mradi huo umetekelezwa kwa muda wa miaka mitatu tangu 2012/13 -2014/15 ambapo umekamilika mwezi Septemba 2014.

Amesema ili kuufanya mradi huo kuwa endelevu wamejenga nyumba ya mlinzi ili kulinda chanzo hicho cha maji kisiharibiwe kwa namna yoyote ile ikiwa ni pamoja na kulinda mazingira yanayozunguka eneo hilo.

No comments:

Post a Comment