Kushoto ni mtaalamu wa magonjwa ya
mfumo wa mkojo na uzazi, Dk.Rajagopal, na upande wa kulia ni mtaalamu wa
magonjwa ya figo, Dk. Sanjay Maitra, walipokuja kuona na kutoa tiba kwa
wagonjwa katika kliniki iliyofanyika hosipital ya Hindu Mandal.
Kuishi ni jambo moja. Kuishi
maisha yenye afya njema ni kitu kingine kabisa. Hakuna anaeweza
kushuhudia juu ya ukweli huu zaidi ya wale wapatao adha itokanayo na
athari za magonjwa yasiyo ya kuambukiza.
Idadi kubwa ya watanzania watu
wazima na watoto wasio na hatia ndio waathirika wanaopata mateso
makubwa kutokana na aina mbalimbali ya magonjwa yasiyo ya kuambukizwa
ikiwa ni pamoja na magonjwa ya moyo, ugonjwa wa kisukari, magonjwa ya
mfumo wa mkojo, magonjwa ya figo, mifumo ya neva, uti wa mgongo na
magonjwa mengine yanayohusiana na haya.
Kwa bahati mbaya, licha ya mipango
mikakati ya kupambana na Magonjwa yasiyo ya kuambukizwa nchini Tanzania,
watanzania wengi bado wanaathirika na kufa kupitia magonjwa haya.
Kulingana na takwimu za hivi
karibuni Shirika la Afya Duniani (WHO), idadi ya vifo vitokanavyo na
magonjwa ya figo nchini Tanzania imefikia 4533 sawa na asilimia 1.03 ya
vifo vyote kwa jumla, wakati kiwango cha maambukizi ya ugonjwa wa figo
katika Tanzania imeripotiwa kuwa katika asilimia 14 .
Sababu kuu ya vifo kwa wagonjwa hawa ni kushindwa kwa figo na mishipa ya moyo au madhara yatokanayo na matatizo hayo.
Kujenga mipango endelevu ya
matibabu kwa wagonjwa wa figo, moyo, kisukari, mfumo wa mkojo, mfumo wa
neva na uti wa mgongo inaendelea kuwa changamoto nchini Tanzania.
Shirika la Afya Duniani
linapendekeza kwamba, nchi zote zinatakiwa kuwa na mtaalamu wa mfumo wa
neva na uti wa mgongo (neurosurgeon) mmoja kwa kila wakazi 100,000. Hii
ni tofauti nchini Tanzania kwani uwiano ni 1: 13,000,000.



No comments:
Post a Comment