Hotel
Za Double Tree By Hilton Tanzania, Tarehe 18.10.2014 walidhamini Siku Ya
Maonesho Ya chakula, yalliyofanyika kwenye viwanja vya shule ya Tanganyika
International Schools. Pichani
Juu Katikati ni Meneja Masoko wa Hotel za Double Tree By Hilton, Bw.
Florenso Kirambata, kushoto ni mpishi mkuu wa Double Tree, Hassan na kulia
ni Ayman.
Akielezea madhumuni ya kuandaa siku hiyo
Mkurugenzi wa Mauzo wa Hotel za Double Tree By Hilton Tanzania, Bw.
Florenso Kirambata; alisema kuwa nia yao kubwa ni kuweza kuzipatia fursa
makampuni mbali mbali na wajasiliamali wadogo wadogo kuweza kuonyesha
uwezo wao na bidhaa wanazotengeneza.
Mr
Florenso akaongeza kuwa zaidi ya wajasiriamali wadogo wadogo 100(mia
Moja) na Wakubwa 50(hamsini) walishiriki kwenye maonesho hayo hasa lengo
kuu ikiwa ni kuonesha aina mbali mbali za vyakula wanavyozalisha hivyo
kuweza kujitangaza na kufahamika
Mpishi
Msaidizi wa Hotel ya Double Tree, Awadh (kushoto), akiwa Anapata
maelekezo toka kwa Mpishi mwenzake, Ayman, namna ya kuandaa na kuchanganya
vyakula
Mpishi Mkuu wa Hotel za Double tree, Bw. Hassan, akitoa maelekezo kwa wasaidizi wake
Meneja
Masoko wa Hotel za Double Tree By Hilton, Bw. Florenso Kirambata, akiwa
na wapishi wa Hotel za Double Tree, wakipata maelekezo kwa mmoja wa
washiriki wa maonesho ya chakula
Wapish wa Hotel Za Double Tree Wakiangali moja ya Bidhaa Toka kwa mshiriki wa maonesho ya siku ya chakula
Mwaandaaji mku wa Maonesho hayo wa kwanza Kulia akiwapa maelekezo wapishi wa Hotel za Double Tree
Mpishi
msaidizi wa Hotel za Double Tree, akiwapa maelekezo wateja waliotembelea
banda lao namna chakula cha Hot Dog kinavyotengenezwa
Banda la American Garden, walikuwepo nao kuonyesha bidhaa zao tofauti tofauti
No comments:
Post a Comment