Mkurugenzi
wa Utawala na Rasilimali Watu, Bw. Barnabas Ndunguru, akimkaribisha mgeni
rasmi ambaye ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na
Michezo, Bi. Sihaba Nkinga (hayupo Pichani), katika ufungaji wa mafunzo
elekezi kwa watumishi wapya wa Wizara. Hafla hiyo ilifanyika hivi
karibuni Jijini Dar es Salaam.
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bi. Sihaba Nkinga,
akiongea na baadhi ya Watumishi wapya wa Wizara katika ufungaji wa
mafunzo elekezi yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam, ambapo aliwaasa kuwa
na maadili katika utendaji wao wa kazi.
Katibu
Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Bi. Sihaba Nkinga,
katikati akiongea na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana, Bw. Leonard
Thadeo (kulia), na Mkurugenzi wa Maendeleo ya Utamaduni, Prof. Hermens
Mwansoko (kushoto), mara baada ya kufunga mafunzo elekezi kwa watumishi
wapya wa Wizara
No comments:
Post a Comment