KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 30, 2014

PSPF YATOA MSAADA WA MABATI 300

unnamed
Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Gerald Guninita, akipokea msaada wa mabati 200, kutoka kwa mwakilishi wa PSPF, kutoka makao makuu, Amelia Rwemamu, kwa ajili ya ujenzi wa maabara za sayansi katika shule za sekondari Wilayani humo, Makabidhiano yalifanyika juzi katika ofisi za Wilaya ya Kilolo
 
Na Mwandishi wetu.
 
KATIKA kutekeleza maagizo ya Rais Jakaya Kikwete, kila shule iwe na maabara tatu ifikapo Novemba mwaka huu, Mfuko wa Pensheni ya Watumishi wa Umma (PSPSF), umetoa msaada wa mabati 300 yenye thamani ya zaidi ya Sh Milioni sita, katika Wilaya za Kilolo na Mufindi, Mkoani Iringa, kufanikisha ujenzi wa maabara hizo na hosteli kwa Chuo cha Ualimu Mufindi.

Wakati Wilaya ya Kilolo imepata bati 200 zitakazotumika kusaidia kukamilisha ujenzi wa maabara unaoendelea  katika shule zake za Sekondari, Chuo cha Ualimu Mufundi (MUTCO), kilichopo Mjini Mafinga Wilayani Mufindi, kimepata bati 100 ikiwa ni kutimiza ahadi iliyotolewa na Meneja wa Sheria wa PSPF, Abrahamu Siyovelwa, aliyotoa May 27 katika mahafali ya chuo hicho.
 
Akikabidhi msaada huo kwa mkuu wa Wilaya ya Mufindi, Monica Kalalu, juzi katika viwanja vya Chuo cha Ualimu Mufindi (MUTCO), Afisa Mfawidhi wa PSPF Mkoa wa Iringa, Baraka Jumanne, alisema lengo la msaada huo ni sehemu ya mpango wao katika kusaidia sekta ya elimu nchini na kutekeleza maombi yaliyoombwa na viongozi wa Wilaya hizo katika kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Rais Jakaya Mrisho Kikwete, kila shule ya sekondari iwe na maabara ifikapo Novemba mwaka huu.
 
“PSPF ni shirika la mfuko wa pensheni hivyo faida lazima iifikie jamii hasa katika suala la elimu ya za sekondari na msingi hivyo tumeamua kuwapatia mabati 100 Chuo cha Mufindi na Wilaya ya Kilolo mabati 200, kutekeleza maombi yao kwa shirika la PSPF kusaidia ujenzi wa maabara na ujenzi wa hostel kwa chuo cha MUTCO hivyo leo tunawakabidhi madawati haya mia tatu kwa lengo la kutekeleza ahadi ya shirika.” Alisema Jumanne.

Aidha Jumanne alitoa wito kwa viongozi kuwashawishi wafanyakazi Kilolo  na wanafunzi wa chuo cha Ualimu Mufindi kujiunga na mfuko wa pensheni kwa watumishi wa umma (PSPF), kwa huduma bora na mafao bora yakiwemo mafao ya uzeeni, ulemavu, mirathi, mafao ya rambirambi za mazishi, malipo ya wategemezi na malipo ya penshini ya kila mwezi.
 
Alitoa faida ya kujiunga na PSPF kwa kuwa kuna baadhi ya mafao mbalimbali yanayotolewa na mfuko huo yanalenga kuwawezesha watumishi kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazowakabili katika utumishi wao kabla na baada ya kustaafu
 
Aliongeza kuwa, PSPF ina mpango imejiwekea mahususi wa kuhakikisha unaboresha maisha wa wanachama wake wakiwemo wasio wafanyakazi, kwa kuweka akiba isiyo ya hiyari itakayowawezasha kufaidika kwa faida ya maisha yao.

Kwa upande wake Mkuu wa Milaya ya Mufindi, Monica Kalalu, alilishukuru shirika la PSPF kwa msaada huo, na kutoa wito kwa wanafunzi na walimu na kuwataka wadau wengine wajitokeze kuisaidia sekta ya elimu hususani ujenzi wa maabara ambao unaendelea nchi nzima kwa sasa,
 
Naye Mkuu wa Wilaya ya Kilolo, Gerald Guninita, alisema kuwa msaada huo utazisaidia shule za sekondari za wilaya ya Kilolo katika kukamilisha ujenzi wa maabara na kuwataka pspf wasiishie hapo katika kutoa msaada zaidi katika sekta ya elimu.
 
Na Amelia Rweyimamu ambaye ni Muwakilishi wa PSPF makao makuu Dar es salaam, akizungumza wakati wa kukabidhi bati hizo alisema kuwa PSPF inatambua umuhimu wa kuwepo kwa maabara hapa nchini hivyo ofisi yake imeona vyema kushiri katika ujenzi huo kwa kutoa bati hizo.
 
Rweyimamu alisema PSPF inatoa mafao mbalimbali ikiwa ni pamoja na fao la uzeeni, fao la ulemavu, fao la kifo, fao la mazishi, fao la wategemezi lisilo na kikomo, fao la kujitoa, fao la uzee, fao la kufukuzwa kazi, na fao la ujasiriamali.
 
Aidha aliongeza kuwa PSPF, inatoa fao la elimu ambapo mfuko hudhamini mikopo katika bodi ya mikopo ya wanafunzi, lengo kubwa ikiwa ni kujenga uwezo wa kuhudumia wanafunzi wengi katika taaluma mbalimbali ikiwemo pia taaluma ya sayansi, Teknolojia na Afya.

No comments:

Post a Comment