KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

October 30, 2014

WANAUME WATAKIWA KUSHIRIKI KATIKA MASUALA YA AFYA YA UZAZI

index

Na Mwandishi wetu.

Wanaume wametakiwa kushiriki katika masuala ya afya ya uzazi, ili waweze kusaidia katika ukoaji wa maisha ya mama na mtoto wakati wa kujifungua.

Kauli hiyo imetolewa leoJjijini Dar es salaam na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinisia na Watoto, Dkt. Pindi Chana, wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Uzazi na Malezi bora Tanzania (UMATI).

Kauli mbiu ya mkutano huo ni miaka 55 ya kutoa huduma bora za uzazi wa mpango Tanzania, ni tumia uzazi wa mpango, okoa maisha.
  Amesema katika kusherekea maika 55 ya UMATI, ni vema wadau wote washirikiane na wataalamu wa sekta ya afya katika kutekeleza kazi zinatokana na hali halisi ya mahitaji ya huduma ya afya ya uzazi kwa jamii hususani kwa wanawake, watoto na vijana ili kuokoa maisha ya wananchi.

Dkt. Chana amesema kuwa, takwimu kwa Tanzania zinazonyesha kuwa vifo vinavyotokana na uzazi ni takribani 454 kwa kila vizazi hai 100,000 .
  Ameongeza kuwa idadi hiyo inaweza kupungua iwapo huduma bora, taarifa sahihi na elimu kuhusu afya ya uzazi itawafikia Watanzania wengi, ili liwe taifa lenye uelewa mkubwa kuhusu masuala ya uzazi.

Dkt. Chana ametoa wito kutumia njia ya makundi  rika  kama mabaraza ya watoto, vilabu vya watoto na vyama vya FEMATALK, ili kufikisha ujumbe kwa ajili ya kuokoa maisha ya mama na mtoto.

Amewataka wajumbe wa mkutano huo kuendelea na juhudi za kuhamasisha jamii ili kuondoa vitendo vya ubaguzi wa kijinsia kama vile ndoa za utotoni na wanaume kutoshiriki katika masuala ya afya ya uzazi sawa na wanawake.

Dkt.Chana ametoa wito kwa UMATI kuendelea na juhudi hizo katika harakati za kumukomboa mtoto wa kike.

No comments:

Post a Comment