Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt.
Asha Rose Migoro (kulia), akimkabidhi cheti Kaimu Balozi wa Japan
nchini, Kazuyoshi Matsu Naga, ikiwa ni ishara ya kutambua msaada wa
nchi hiyo wa kuisaidia Shule ya Sekondari ya Wasichana wanaoishi
katika mazingira hatarishi ya WAMA Nakayama iliyopo katika kijiji cha Nyamisati, Wilayani Rufiji Mkoani Pwani, wakati wa sherehe ya mahafali ya pili
ya shule hiyo yaliyofanyika jana.
Na Mwandishi wetu.
UBALOZI wa Japan kupitia Wizara
ya Mambo ya Nchi za Nje, umetoa kiasi cha fedha cha Sh. Milioni 800,
ambazo ni sawa na Dola za Kimarekani 500,000 kwa ajili ya kusaidia Shule
ya Sekondari ya Wasichana wanaoishi katika mazingira hatarishi ya
WAMA Nakayama, iliyopo wilayani Rufiji mkoani Pwani.
Hayo yalisemwa jana na Kaimu Balozi wa Japan chini, Kazuyoshi Matsu Naga, wakati wa sherehe za mahafali ya pili ya shule hiyo, yaliyofanyika jana na kuhudhuriwa na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Asha Rose Migiro, ambaye alikuwa mgeni rasmi. Baadhi ya viongozi wakiwemo baadhi ya wake za viongozi na wageni wengine mbalimbali.
“Juzi Idara ya Mambo ya nje ya Japan, ilikubali kutoa Dola
za Marekani 500,000 kwa ajili ya mradi mpya wa awamu ya pili wa
kusaidia shule ya Sekondari ya WAMA Nakayama,” alisema Kaimu Balozi
huyo.
Matsu Naga aliongeza kwamba, fedha hizo zitatumika kwa ajili ya ujenzi wa jengo la kompyuta na utawala, yakiwemo mafunzo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).
“Sisi Wajapan, tunapenda kuendelea kutoa msaada kadri
inavyowezekana. Msaada wa leo utaongeza urafiki kati ya nchi ya Japan na
Tanzania,” alisisitiza.
Kaimu Balozi huyo alimataka kila wanafunzi wa shule hiyo, kutoa
mchango wake katika kuleta maendeleo ya jamii kwa kutumia mafunzo
aliyoyapata.
Kwa upande wake, Dkt. Migiro, ambaye alikuwa mgeni rasmi katika sherehe hizo, aliwataka wadau mbalimbali kuendelea kumsaidia Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Salma Kikwete, katika kusaidia wanafunzi hao ili kupanua fursa za watoto wa kike kielimu.
“Nimegundua kuwa mtoto wa kike wanakabiliwa na upungufu wa
fursa kitaaluma. Hivyo kuchangia shule hii kwa mtoto wa kike ni kujenga
na kuihimarisha fursa yake yeye binafsi na familia kwa ujumla.
Dkt. Migiro alifurahishwa uweledi wa wanafunzi wa shule hiyo,
yakiwemo mazingira bora, ambapo alisema shule hiyo inaviwango bora.
Naye Mke wa Rais Mama Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa
Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA), aliwataka wanafunzi hao
kutumia nafasi ya kusoma kwa bidii ili waweze kufaulu hatimaye kushika
nafasi mbalimbali za uongozi kama Dkt.
Akizungumzia kuhusu matarajio ya WAMA kutokana shule hiyo,
alisema kutoa wataalamu wa nyanja zote, ikiwemo fani ya sayansi.
Hivyo aliwataka kuongeza bidii katika masomo ya sayansi.
Alisema WAMA itaendelea kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu hadi watakapofikia hatua ya mwisho.
Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa
na Serikali za Mitaa Tamisemi (TAMISEMI), Hawa Ghasia, aliwapongeza walimu
wa shule hiyo kwa bidii zao ambazo zimeifanya shule hiyo kuongoza
katika Wilaya hiyo.



No comments:
Post a Comment