Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF) na Klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), wamekutana mwishoni
mwa wiki na kujadili masuala mbalimbali ya kuboresha maendeleo ya
mchezo huo nchini.
Mkutano huo uliofanyika Dar es
Salaam uliongozwa na Rais wa TFF, Jamal Malinzi, na kuhudhuriwa na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF pamoja na Wanyeviti wa klabu za
VPL.
Masuala yaliyozungumzwa ni leseni
za klabu (club licensing), maboresho ya Taifa Stars, Kanuni za Ligi Kuu,
Kombe la FA (Shirikisho) na mchango wa klabu hizo katika kuendeleza
mpira wa miguu kwa vijana.
Uwasilishaji katika mkutano huo
kuhusu maboresho ya Taifa Stars ulifanywa na Kocha Mkuu wa timu hiyo
Mart Nooij wakati leseni kwa klabu ulifanywa na Mkurugenzi wa Mashindano ya TFF, Boniface Wambura.
Kuhusu Kombe la FA, klabu
zilifahamishwa kuwa mazungumzo kati ya TFF na mdhamini yanaendelea,
ambapo zilikaribisha wazo hilo kwa vile michuano hiyo itatoa fursa kwa
timu zao kucheza mechi nyingi za mashindano, hivyo kutoa nafasi ya
kucheza kwa wachezaji wengi zaidi.
Bingwa wa michuano ya FA ndiye atakayeiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Kombe la Shirikisho barani Afrika.
Rais Malinzi, aliziomba klabu
kukutana na kuwasilisha mapendekezo yao ya jinsi ya kuchangia/kuboresha
maendeleo ya mpira wa miguu kwa vijana, kuboresha Kanuni za Ligi Kuu na
kuboresha Kanuni za Bodi ya Ligi ili yaweze kufanyiwa kazi.
No comments:
Post a Comment