Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF) linakaribisha wabunifu, kubuni mwonekano wa jezi mpya za
timu ya Taifa kwa mechi za nyumbani na ugenini. Ubunifu ni lazima
uzingatie rangi za bendera ya Taifa.
Mshindi wa jezi ya nyumbani
atapata sh. 1,000,000 (milioni moja), na mshindi wa jezi ya ugenini
atapata pia sh. 1,000,000 (milioni moja).
Ubunifu utumwe kwenye anwani ya barua pepe: info@tff.or.tz
au uwasilishwe kwa CD au flash zikiwa katika mfumo wa PDF katika ofisi
za TFF zilizopo ghorofa ya tatu katika Jengo la PPF Tower, Mtaa wa Ohio
na Garden Avenue. Mwisho wa kupokea designs ni Novemba 15, 2014.
Kwa maelezo zaidi unaweza kuwasiliana nasi kwa simu namba; 0713 210242 au 0714 634838.
No comments:
Post a Comment