Na Mwandishi wetu.
WANANCHI wameshauriwa kuisoma
Katiba Mpya Inayopendekezwa sura kwa sura na ibara kwa ibara, ili waweze
kupata uelewa wa masuala mbalimbali yaliyomo ndani ya Katiba hiyo na
kuacha kusikiliza maneno ya watu yenye nia ya kupotosha ukweli.
Kauli hiyo ilitolewa jana na
Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Asha Rose Migiro, wakati wa sherehe za
mahafali ya pili ya Shule ya Sekondari ya Wasichana wanaoishi katika
mazingira hatarishi ya WAMA Nakayama, iliyopo Wilayani Rufiji Mkoani
Pwani.
Dkt. Migiro, ambaye alikuwa
mgeni rasmi katika sherehe hiyo, ambayo ilihudhuriwa na baadhi ya
viongozi, wakiwemo baadhi ya wake za viongozi na wageni wengine
mbalimbali.
“Nchi yetu ilikuwa katika mchakato wa uandikaji wa Katiba Inayopendekezwa kazi ambayo ilikamilika Oktoba 8, mwaka huu.
“Tusikubali kusomewa na tutakapokamilisha kazi ya kuisoma tuipigie kura ya ndiyo,” alisema Dkt. Migiro.
Akizungumza na katika mkutano wa
mabalozi wanazoziwakilisha nchi zao katika Jamhuri ya Watu wa China
uliofanyika kwenye Nyumba ya kufikia Wageni ya Serikali ya Diaoyutai,
Beijing, Rais wa Jakaya Kikwete alisema, Kura ya Maoni inatarajiwa
kupigwa wakati wowote Aprili mwaka ujao kama mambo yataenda vizuri.
Rais Kikwete alikabidhiwa Katiba hiyo hivi karibuni mjini Dodoma, baada ya Bunge Maalum la Katiba kumalizia kaze yake.



No comments:
Post a Comment