Mzozo
mkubwa umesababisha Bunge la Tanzania kuvunjika usiku wa jana wakati
likiendelea na mjadala wa kashfa ya Escrow, baada ya wabunge kushindwa
kukubaliana njia sahihi ya kuwawajibisha baadhi ya viongozi wa kisiasa
wanaotuhumiwa kuhusika na sakata la wizi wa Zaidi ya fedha za Tanzania
shilingi bilioni 300 kutoka Benki Kuu ya nchi hiyo.
Taarifa ya
mwandishi wa BBC Baruan Muhuza imesema kuwa Bunge hilo, jana limeweka
rekodi ya kuwa na mjadala wa muda mrefu Zaidi kuliko wakati mwingine
wowote. Hadi kufikia kuvunjika kwa kikao hicho ilikuwa ni saa 4.30 usiku
kwa saa za Afrika Mashariki. Spika wa Bunge hilo Anne Makinda karibu
muda wote wa kikao hicho alijikuta akitoa tahadhari kwa wabunge wake
kujilinda na hatua za kuingilia mihimili mingine ya utawala ya Tanzania
ambayo ni Mahakama na Serikali. Hatua hiyo kwa namna fulani iliamsha
hisia tofauti kutoka upande wa kambi ya upinzani pamoja na wajumbe wa
kamati ya hesabu za Serikali ambao walitishia kutoka nje hadi viongozi
wanaodaiwa kulindwa na bunge hilo wawajibike wenyewe. Bunge hilo
linategemewa kuendelea na kikao chake hapo leo.
No comments:
Post a Comment