Katibu
Mkuu wa CCM, Ndg. Abdulrahman Kinana akinyanyua mikono juu kuashiria
mshikamano na baadhi ya viongozi wa makundi ya Chama cha SPLM cha Sudan
Kusini ambao wako kwenye mgogoro wa kugombea madaraka kwa takribani
mwaka sasa. Kinana amekutana na viongozi hao wakati wa mkutano wa
hadhara mjini Masasi, Mtwara baada ya kumfuata na kutaka ushauri wa
upatanishi nchini kwao Sudani Kusini. Baada ya viongozi hao kupata
wasaa wa kusalimiana na wananchi katika mkutano huo uliofanyika mjini
Masasi Baadae Kinana alifanya nao mazungumzo Ikulu Ndogo ya Masasi.
Viongozi hao wamemfuata Kinana mjini Masasi kutokana na kwamba yuko
katika ziara ya kikazi ya mikoa ya Lindi na Mtwara akiendelea na
shughuli za kuimarisha Chama hicho na kukagua utekelezaji wa Ilani ya
Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 akiongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC
Itikadi, Siasa na Uenezi
Viongozi wa vikundi hivyo wakiwa mjini katika mkutano wa CCM mjini Masasi
Kinana akizungumza na viongozi hao ikulu ndogo mjini Masasi
Katika
ziara yake inayoendelea mkoani Mtwara Kinana alitembelea kiwanda cha
kubangua korosho na kujieonea shughuli mbalimbali zinazofanywa
kiwandani hapo hapa akionyesha wa mashine ya kufunga korosho.
Baadhi ya akina mama wafanya kazi wa kiwanda hicho wakichambua korosho na kuzitenga katika madaraja
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia mashine za kisasa za kubangua korosho
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza baada ya kukagua kiwanda hicho kinachomilikiwa na mama Kate Kamba. kulia
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Afisa Ushirika wa
Mkoa wa Mtwara Bw. John Henjewele kuhusu matatizo ya korosho kushoto ni
Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki ujenzi wa Makaravati katika barabara ya Migongo mjini Masasi
No comments:
Post a Comment