Meneja
wa NHC Mkoa wa Tabora, Erasto Chilambo, akiwasilisha ripoti ya
utekelezaji wa mradi wa nyumba za gharama nafuu za NHC Isikizya, zilizopo Wilayani Uyui Mkoani Tabora, kwenye semina ya Mameneja na Wakurugenzi
wa NHC inayoendelea katika Hoteli ya Tanga Beach Resort.
Meneja wa NHC Mkoa wa Dodoma,
Itandula Gambalagi, akiwasilisha ripoti ya utekelezaji wa mradi wa nyumba
za gharama nafuu za NHC Mnyakongo, Kongwa Dodoma, kwenye semina ya
mameneja na wakurugenzi wa NHC inayoendelea katika Hoteli ya Tanga Beach
Resort.
Washiriki wa Semina hiyo
Wenceslaus Tillya, Meneja wa NHC mkoa wa Temeke, Nehemia Msigwa, Meneja
wa NHC Katavi na Daniel Nkya wakifuatilia kwa kina somo lililokuwa
likitolewa na Wataalamu
Washauri wa Delloite Touche juu ya mapitio ya Mpango Mkakati wa Shirika
unaomalizika mwakani, ili kuuboresha kwa kipindi kijacho. Somo hilo
lilitolewa kabla ya mawasilisho ya mameneja wa mikoa.
Meneja
Mshauri Taasisi inayojishughulisha na mambo ya uchumi
ya Deloitte, Bw.Frederick Nsemwa, Mkurugenzi wa Watushi Housing Limited,
Dk Fred Nsemwa, na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu, wakifuatilia somo hilo
Wataalamu washauri wa semina hiyo
wakiwa pamoja na Mkurugenzi wa Rasilimaliwatu, James Rhombo, na
Mkurugenzi wa Uendelezaji Miliki Benedict Kilimba, wakifuatilia semina
hiyo.
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Huduma kwa Jamii, Susan Omari akifuatilia kwa kina soma hilo la Delloite Touche.
Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi wa
Ndani, Fatuma Chillo, akisisitiza jambo katika semina hiyo huku
Mkurugenzi wa Fedha, Felix Maagi, na Mkurugenzi wa Uendelezaji Biashara,
David Shambwe, wakifuatilia.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa, Nehemia Kyando Mchechu, akisisitiza jambo katika semina hiyo.
Washiriki wakifuatilia mada iliyotolewa na Wataalamu wa Afrika Kusini kutoka kampuni ya Hydraform.
Wataalamu wa Afrika Kusini kutoka kampuni ya Hydraform, wakiwa na mdau kutoka Hydraform Tanzania wakifuatilia semina hiyo
No comments:
Post a Comment