KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

November 25, 2014

WATEJA WA TIGO KULAMBA BILIONI TATU

index
Tigo imetangaza leo kwamba imetoa malipo yake ya kwanza ya kila robo mwaka ya kiasi cha shilingi bilioni 3 (dola milioni 1.8) kwa wateja wake wa Tigo Pesa. Mgao huu ni wa kwanza kati ya awamu nne za malipo zinazotarajiwa kufanyika kila mwaka. Malipo haya yanafanyka miezi mitatu baada ya kampuni hiyo kulipa kiasi cha shilingi bilioni 14.25 (dola milioni 8.64) ambacho kilikuwa kimelimbikizwa katika mfuko wa fedha ya akaunti ya Tigo Pesa, malipo yaliyoifanya Tigo kuwa kampuni ya simu ya kwanza duniani kuwagawia faida watumiaji wake wa huduma ya fedha kwa simu za mkononi. Tigo Pesa ina jumla ya watumiaji milioni 3.6. Meneja Mkuu wa Tigo Diego Gutierrez alisema, “Hii duru ya pili ya kutoa gawio ni udhihirisho tosha wa muendelezo wa kampuni yetu katika kuwanufaisha wateja na kuboresha maisha ya Watanzania. Malipo haya yanaenda kwa kila mtumiaji wa Tigo pesa wakiwemo mawakala wakuu, mawakala wa reja reja na watumiaji wa kawaida wa huduma hii. ” “Gawio la kwanza lilikuwa kubwa zaidi kwa sababu faida ilimbikizwa kwa muda wa zaidi ya miaka mitatu na nusu ikilinganishwa na malipo haya ya pili ambayo yanatokana na malimbikizo ya faida ya fedha zilizohifadhiwa katika mifuko ya benki za kibiashara kwa muda wa miezi mitatu t kutoka Julai hadi Septemba 2014,” alisema Meneja Mkuu huyo. Gutierrez alieleza kwamba, kama ilivyokuwa hapo awali, malipo wanayopata wateja awamu hii yanatokana na salio lao la kila siku kwenye akaunti zao za Tigo Pesa. Hii ni kwa wote; mawakala wakuu, mawakala wa reja reja na watumiaji wa kawaida. Mgao unaofuata wa mwezi Oktoba mpaka Desemba 2014 utalipwa mwezi Februari 2015. Kuhusu Tigo: Tigo Tanzania ni kampuni ya mawasiliano inayoongoza kwa ubunifu nchini, inafahamika kama kampuni inayolenga kuleta maisha ya kidijitali katika jamii. Inatoa huduma tofauti tofauti za mawaliano kwa njia ya simu, intanet ya kasi na kutuma na kupokea fedha. Aidha Tigo imebuni bidhaa na huduma mbali mbali kama Facebook kwa Kiswahili, Tigo Pesa App kwa watumiaji wa simu za Android na iOS, na ni kampuni ya simu ya kwanza Afrika Mashariki kuanzisha huduma ya kutuma na kupokea pesa kwa njia ya simu kimataifa, yenye uwezo wa kubadilisha fedha za kigeni. Kwa kutumia tekinolojia ya 3G Tigo ina wahakikisha wateja upatikanaji wa huduma bora na za uhakika. Kati ya mwaka 2013 na 2014, kampuni ilizindua minara mipya zaidi ya 500 na pia ina mipango wa kuongeza mara mbili kiwango cha uwekezaji ifikapo mwaka 2017 ili kuweza kupanua wigo wa mawasiliano na uwezo wa mtandao hasa hasa katika maeneo ya vijijini. Tigo ina wateja zaidi ya milioni 7 na inatoa ajira za moja kwa moja na kwa namna mbali mbali kwa Watanzania zaidi ya 100,000 ambao wanajumuisha wafanyakazi wa huduma kwa wateja, wa kutuma na kupokea fedha, watu wa mauzo pamoja na wasambazaji. Tigo ni kampuni ya simu inayoongoza chini ya kampuni mama ya mawasiliano Millicom, ambayo imejizatiti katika kuhamasisha na kufanikisha maisha ya kidijitali katika nchi 44 zenye biashara zake Afrika na Latin Amerika, pamoja na ofisi za kampuni zilizopo Ulaya na Marekani. Kwa kutambua kwamba ubunifu ndio utakaowafanya kuendelea kuwa juu ya ushindani, Millicom inaendelea kuthamini mchango wa wadau wake, wakitumia dhana ya “demand more” kama namna ya kufanya biashara na kuendeleza nafasi yao kama kampuni inayoongoza katika kufanikisha maisha ya kidijitali katika baadhi ya masoko makubwa yenye ushindani mkali duniani.

No comments:

Post a Comment