KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 30, 2015

26 WAUAWA KIGAIDI MISRI

 Gari la kivita la Serikali nchini Misri

Takriban watu 26 wameuawa katika mfululizo wa mashambulizi yaliyofanywa na kundi la wapiganaji la Islamic State Kaskazini mwa Misri katika eneo Sinai
Gari lililokuwa na mabomu lilipiga kituo cha kijeshi kaskazini mwa Sinai katika mji wa El-Arish na kuwaua wanajeshi kadhaa. Mashambulizi mengine kama hayo yalifanyika katika mji jirani Sheik Zuwayid na mji wa Rafah katika mpaka wa Gaza.
Kundi la wapiganaji la Ansar Beit al-Maqdis ambalo ni mshirika wa wapiganaji wa Islamic State wamekiri kutekeleza shambulio hilo.
Maafisa wa jeshi nchini Misri wanasema gari hilo lililokuwa na mabomu liliegeshwa nje ya ngome ya jeshi ya El-Arish na mashambulizi yake yalilenga hoteli ya jeshi na maeneo mengine mhimu katika kituo hicho.
Hata hivyo kundi hilo lilianza kutekeleza mashambulizi yake nchini Misri tangu kuangushwa kwa utawala wa Rais aliyekuwa na msimamo mkali wa Kiislam Mohammed Morsi mwaka 2013.
Hofu imetawala katika miji kadhaa nchini Misri wiki hii kutokana na sherehe za kumbukumbu za kuangushwa kwa utawala wa aliyekuwa Rais wa Taifa hilo na aliyeondolewa madarakani mwaka 2011 Hosni Mubarak -BBC

No comments:

Post a Comment