KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 24, 2015

BAADA YA KUWA KIPORO KWA MUDA MREFU, HATIMAYE PROF.MUHONGO AACHIA NGAZI MWENYEWE



Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo

WAZIRI wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo amejiuzulu nafasi yake baada ya kile alichosema ni kuandamwa kila kona kuhusu sakata la Akaunti ya Escrow huku akisisitiza kuwa yeye hahusiki hata kidogo na kashfa hiyo.Akizungumza na waandishi wa habari mda mfupi uliopita, Profesa Muhongo alisema ameamua kuchukua uamuzi huo baada ya kushauriana kwa kina na Rais Jakaya Kikwete pamoja na familia yake.Amesema kashfa ya Escrow imemdhalilisha yeye na familia yake ilhali hahusiki na kumtaka mtanzania yeyote mwenye ushahidi aupeleke mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEib4s10THkoynOysl-Hq-ozgMsuUPc4lH3p97dBmapNMduQCuymQbGQcwmsJcavWn1ioNxC4KlvHUXLCZWJ3RolM5jRNLeTpQnzzLYkFSb-Eb4SE8cIgoqpXi0p1Hpyg9e8QHxs5Qs50vI/s1600/DSCF1860.jpg
Alivyokuwa ana bwaaga manyanga
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjbeqJzO4W0w6LzyD8nc96h_QYs6cWeOC5EBNwGy3t07mti-z86RDviE52u3SIrPhSfnU8xKu1-zwnQYC55-Z6UFknmOg-tuAtwMnqk9hWx7iD2sGVTfWKPDLAJfGD5ZM64vLEFPVo34vc/s1600/DSCF1873.jpg
Sehemu ya wanahabari waliohudhuria mkutano huo wa kubwaga manyanga
Ametaja sababu nyingine ya kujiuzulu kwake kuwa ni kukisaidia chama chake (CCM), ili kurudisha imani ya wananchi kwa chama hicho na serikali kwa ujumla kutokana na kuadhibiwa chama badala yake.Kujiuzulu kwa Profesa Muhongo yumkini kukakamilisha tamthiliya ndefu ya kashfa ya Escrow kwa kuwa watuhumiwa wote wa sakata hilo waliopendekezwa na bunge wamewajibishwa au kuwajibika.Sakata la Akaunti ya Escrow lilisababisha kujiuzulu kwa Mwanasheria Mkuu wa serikali, Fredirick Werema kwa kushindwa kuishauri vizuri serikali kuhusu fedha za akaunti hiyio, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijukana kutokana na kupokea mgao wa fedha hizo, pamoja na wenyeviti wa kamati za Bunge Andrew Chenge, Victor Mwambalaswa na Wiliam Ngeleja pia kwa kupokea mgao wa fedha hizo.                                               

No comments:

Post a Comment