KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 24, 2015

WATU BWANA, HATA NDEGE MNAKODI MBOVU SASA INGEHARIBIKA ANGANI INGEKUWAJE?

Pg 3
KAMATI ya Bunge ya Hesabu za Serikali na Mashirika ya Umma (PAC), imeagizwa kufikishwa mahakamani kwa watumishi wa Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) waliohusika na mkataba wa ukodishaji ndege mbovu.
Akizungumza wakati wa kuhitimisha taarifa ya PAC kwenye kikao kilichopokea taarifa ya ATCL, Mwenyekiti wa kamati hiyo, Zitto Kabwe, alisema ukodishwaji wa ndege kutoka Kampuni ya Wallis Trading Inc. ya China kulikofanywa na wataalamu wa Tanzania kuliisababishia serikali deni la dola milioni 42.4.
Alisema hadi sasa waliofanya madudu hayo hawajachukuliwa hatua, wakati serikali inalipa hasara hiyo kuanzia Oktoba mwaka jana na kwamba hadi sasa imekwishalipa dola milioni 26.1.
“Utaratibu huu wa kuwaacha watu wanaohujumu waendelee na utumishi serikalimi haufai kwa sababu watakuwa wanafuja fedha za umma wakijua hakuna hatua yoyote itakayochukuliwa dhidi yao,” alisema Zitto.
Akirejea historia ya tukio hilo, alisema Kampuni ya Wallis ilisaini mkataba na ATCL Oktoba 2007 wa ukodishwaji wa ndege kwa kipindi cha miaka sita kwa malipo ya dola 370,000 kila mwezi, ikiwa ni gharama za kukodi ndege na Serikali iliridhia kutoa dhamana.
Alisema baada ya ndege kuwasili ilifanya kazi kwa kipindi cha miezi sita tu na ilipofika Desemba 2008, Mamlaka ya Usafiri wa Anga iliifungia ATCL kwa kushindwa kutekeleza matakwa ya usafiri wa anga, ikiwemo kurekebisha vitabu vinavyoeleza mambo ya usalama wa ndege.
Alisema ndege hiyo ilipelekwa Mauritania kwa ajili ya matengenezo ya kawaida mwezi Machi mwaka 2009 na ilipofika Julai 2009 ilipelekwa Ufaransa kwa ajili ya matengenezo makubwa baada ya kutimiza miaka 12 tangu ilipotengenezwa kwa mujibu wa taratibu za matengenezo ya ndege.
Zitto alisema mkataba wa ukodishwaji na matengenezo yote yalipaswa kufanywa na ATCL, lakini kwa sababu ya hali mbaya ya kifedha ya serikali, ndege hiyo ilishikiliwa na aliyeifanyia matengenezo hadi mkataba wa ukodishwaji ulipovunjwa Oktoba 11 mwaka 2011.
“Mbaya zaidi Wallis alimwandikia Mwanasheria Mkuu wa Serikali kumweleza nia ya kutaka kuishtaki Serikali kwa kushindwa kulipa deni hili.

No comments:

Post a Comment