KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 24, 2015

BREAKING NEWS! RAIS KIKWETE AFANYA MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI LEO

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhsEelNICw_N1fZHZ02AYDiI3ScU-2SobCY-RhXKH8deaBcNs277buVzAPjf51X__ulnUtjlZCxgGkeynbCn8KqmPtYNe9qYhhkMzimiLMPJgq4QX3uh2XVL4iGcaRz7jcT1nNiYtfYUEU/s1600/WAZIRI+LEO0.jpg
Katibu Mkuu Kiongozi,Ba;ozi Ombeni Sefue akitangaza mabadiliko hayo mbele ya Waandishi wa Habari Jijini leo
 
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amefanya mabadiliko kwenye Baraza la Mawaziri leo.
Akitangaza mabadiliko hayo Katibu Mkuu Kiongozi Ofisi ya Rais,  Balozi  Ombeni Sefue aliwataja Mawaziri hao wapya ambao wanaapishwa jioni hii na Wizara zao kwenye mabano kuwa George Simbachawene (Nishati na Madini), Mary Nagu (Mahusiano na Uratibu), Dk. Harrison Mwakyembe, (Afrika Mashariki).
Wengine ni Wiliam Lukuvi (Ardhi, Nyumba na Makazi), Steven Wassira (Kilimo Chakula na Ushirika), Samwel Sitta (Uchukuzi), Jenista Mhagama (Sera na Uratibu wa Bunge) na Christopher Chiza (Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji na Uwezeshaji).
Rais pia ameteua Manaibu Waziri na Wizara zao kwenye mabano kama ifuatavyo: Steven Masele (Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano), Angellah Kairuki (Ardhi Nyumba na Makazi), Ummy Mwalimu (Katiba na Sheria), Anna Kilango Malecela (Elimu na Mafunzo ya Ufundi), Charles Mwijage (Nishati na Madini).

No comments:

Post a Comment