KWA MAONI AU USHAURI E-mail: inocomm2014@gmail.com, PIGA SIMU: 0714555668

www.utt-pid.org


TEMBELEA: www.utt-pid.org

January 23, 2015

DK.HUSSEIN ATEULIWA KUWA MWENYEKITI WA MUDA WA BENKI YA NBC


Displaying Dk hussein.JPG
Dk.Hussein                                                                   
NATIONAL BANK OF COMMERCE
BENKI YA TAIFA YA BIASHARA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Dk Hussein ateuliwa kuwa mwenyekiti wa muda wa Bodi ya Wakurugenzi ya NBC

JANUARI 22, 2015

 Dar es Salaam: Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imemteua Dk Kassim Hussein kuwa mwenyekiti wa muda wa bodi ya wakurugenzi.

Hatua hiyo imetokana na kuteuliwa kwa aliyekuwa mwenyekiti wa bodi ya benki hiyo, Profesa Mussa Assad, kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa hesabu za Serikali (CAG) wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania .

Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari iliyotolewa jijini Dar es Salaam leo, Mkurugenzi Mtendaji wa Muda wa NBC, Bwana Pius Tibazarwa alisema Dk Hussein atashika wadhifa wa uenyekiti wa bodi ya benki hiyo mpaka pale atakapoteuliwa mwenyekiti wa kudumu wa bodi hiyo.

Dk Hussein ni mhadhiri mwandamizi katika masomo ya kibenki na ya fedha katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha (Institute of Finance Management – IFM) cha Dar es Salaam. Dk Hussein ni msomi mwenye Digrii ya Uzamivu katika masomo ya kibenki na Digrii ya Uzamili katika masomo ya fedha. Aliteuliwa kuwa mjumbe wa bodi ya Wakaurugenzi wa NBC tangu mwaka 2010.

“Kwa mara nyingine tena, tunampongeza Profesa Assad kwa kuteuliwa kwake na kumtakia kila la kheri katika kazi hiyo. Tunamshukuru pia kwa utumishi wake uliotukuka katika kipindi chake kama mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi ya NBC. NBC itaendelea kushirikiana nae kuimarisha uwazi na uwajibikaji katika sekta ya fedha hapa nchini. Wakati huo huo, tunamtakia kila la kheri Dk Hussein katika nafasi yake mpya ya uenyekiti wa bodi ya NBC,” alisema Tibazarwa.

Profesa Assad aliteuliwa kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania mnamo mwezi Novemba 2014 baada ya kuitumikia NBC kama mwenyekiti wa bodi tangu mwaka 2006.




No comments:

Post a Comment